UHARIBIFU WA MIFUMO YA CHANZO CHA MAJI MTO KATUMA UNAATHIRI ZAIDI WANYAMA AINA YA VIBOKO.

MUUNGANO   MEDIA
0


 Wakazi wa mkoa wa Katavi wametakiwa kutovamia na kuharibu mifumo ya chanzo cha maji  mto Katuma kwakuwa  kufanya hivyo inaathiri rasilimali za misitu na wanyama hususani viboko.


Akizungumza na Mwananchi leo Alhamis Februari Mosi 2024  Msimamizi wa bonde la maji mto Katuma Mathew Edson amesema changamoto hiyo inasababishwa na baadhi ya watu kuvamia na kuanzisha shughuli za kilimo,ufugaji na ukataji miti ovyo.


“Uharibifu ni mkubwa tunajitahidi kuhifadhi  kwa kutumia Jumuiya zinazoshirikiana na uongozi wa vijiji angalau kwasasa tatizo limepungua,”


“Kidakio cha Katuma kina mito mitatu,mto mama Katuma,Mpanda na Msaginya,tulifanikiwa  kuzibua vibanio haramu 46 vilivyosababisha upotevu wa maji mkubwa,”amesema Edson


Amesema maji hayo yanalikuwa  yanayokwenda mashambani bila mpangilio wowote na kwamba ilisababisha viboko kukosa maji  wakati wa kiangazi.


Mwakilishi Meneja mradi wa Sustain Eco unaofadhiliwa na Ubalozi wa Swiden  ili kuboresha mifumo ya Ikolojia mkoani Katavi Fadhil Njilima amesema wamebaini kuna changamoto kubwa ya  uvamizi wa mito.


“Kuna matatizo makubwa katika maeneo hayo hasa umwagiliaji usio endelevu, uvamizi wa misitu kwaajili ya ufugaji na kilimo usiofuata sheria,”


“Tunachokifanya ni kuielimisha jamii kuona umhimu wa kutunza rasilimali hizo ili mfumo wa  ikolojia ufanye kazi vizuri na uzalishaji uwe endelevu,”amesema Njilima


Baadhi ya wakazi wa mkoa wa Katavi Diana Maico  amesema uelewa wa jamii katika masuala ya uhifadhi upo kiwango cha chini kutona na  ukosefu wa elimu.


“Wanakwenda kulima kwenye maeneo yaliyotengwa kuhifadhia kwa kigezo cha kufuata ardhi yenye rutuba inachangiwa pia na watu kukosa mbinu za kilimo cha kisasa,”


“Hawanunui pembejeo kwa makusudi ama kwa kukosa uwezo au wanataka kulima mashamba makubwa sana ambayo ndani ya kijiji hayapo  wabadilike,”amesema Diana


Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)