MRADI WA KUPELEKA UMEME WA GRIDI RUKWA UMESHAANZA- MHE. KAPINGA

MUUNGANO   MEDIA
0


 Katika jitihada za kuhakikisha maeneo yote nchini yanapata umeme wa uhakika,

Serikali imeshaanza kutekeleza mradi wa kupeleka umeme wa Gridi katika Mkoa

wa Rukwa kupitia mradi wa TAZA ulioanza kutekelezwa mwezi Novemba, 2023

na unatarajiwa kukamilika Mwezi Agosti, 2026.

Hayo yameelezwa leo bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe.

Judith Kapinga wakati akijibu swali la Mbunge wa Nkasi, Mhe. Aida Khenani

aliyetaka kufahamu mkakati wa kumaliza changamoto ya upatikanaji umeme

wilayani Nkasi Mkoa wa Rukwa.

Amesema kuwa, kwa sasa TANESCO inaendelea kufanya maboresho ya

miundombinu ili kupunguza changamoto ya upatikanaji umeme mkoani humo na

kujenga kituo kipya cha kupoza umeme.

Kuhusu hali ya upatikanaji umeme nchini amesema kuwa, upungufu wa umeme

unaendelea kupungua akitaja takwimu kuwa, upungufu umepungua kutoka

megawati 400 hadi 144 kwa siku ya leo.

Ameeleza kuwa, Serikali inaendelea kufanya juhudi mbalimbali ili kuboresha hali

ya upatikanaji umeme nchini akitolea mfano utekelezaji wa Mradi wa umeme wa

Julius Nyerere (JNHPP) ambao inatarajiwa kuwa, katika mwezi wa Pili kuelekea

Machi mwaka huu utaanza kuingiza megawati 235 katika Gridi ya Taifa.

Mhe. Kapinga pia amezungumzia kazi ya upelekaji umeme wa gridi mkoani

Katavi ambapo ameeleza kuwa, tayari kuna mradi unaoendelea kutekelezwa na

kwa sasa baadhi ya vituo vya kupoza umeme vimekamilika na hivyo, nguvu

sasa inawekwa zaidi katika ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kwenda mkoani

humo.

Cap

Moja

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga akijibu maswali mbalimbali ya

Wabunge, bungeni jijini Dodoma tarehe 1 Februari, 2024.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)