Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama ametoa wito kwa wananchi katika maeneo yote ambayo miradi ya maendeleo ya TASAF inatekelezwa, kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) katika kuzuia vitendo vya rushwa ambavyo ndio visababishi vya miradi hiyo kutokamilika kwa wakati na hatimaye kuchelewesha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Mhe. Jenista ametoa wito huo akiwa kwenye ziara yake ya kikazi ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba za watumishi wa Zahanati ya Kijiji cha Ihayabuyaga, Halmashauri ya Wilaya ya Magu mkoani Mwanza inayojengwa na TASAF kupitia ufadhili wa Umoja wa Nchi zinazosambaza Mafuta Duniani (OPEC).
Mhe. Jenista amewasisitiza wananchi kuwa mstari wa mbele katika usimamizi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo ikikamilika kwa wakati inawanufaisha kwa kuwapatia huduma bora kama ilivyokusudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Mhe. Jenista amesema, Serikali imekusudia kila fedha ya mradi inayotolewa, itumike vizuri na ndio maana kupitia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imeanzisha programu maalum ya TAKUKURU RAFIKI aliyoizindua Disemba 20, 2022 jijini Dodoma ikilenga kuwashirikisha wananchi na wadau katika kuzuia vitendo vya rushwa nchini.
“Kupitia TAKUKURU RAFIKI, wananchi wanakuwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya TAKUKURU katika mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa, hivyo tutoe taarifa ya viashiria au uwepo wa vitendo vya rushwa bila woga kwani TAKUKURU RAFIKI ipo kwa ajili hiyo,” Mhe. Jenista amesisitiza.
Mhe. Jenista ameongeza kuwa, hivi sasa TAKUKURU RAFIKI ipo karibu na kila Mtanzania kwa lengo la kuhakikisha kila mradi unatekelezwa vizuri, hivyo ni wajibu wa kila mwananchi kuitumia fursa ya TAKUKURU RAFIKI kulinda fedha za umma zinazotokana na kodi ambazo zinachangiwa na wananchi.
Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Magu mkoani Mwanza, Mhe. Boniventura Kiswaga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan