ARUSHA YAPOKEA TRILION 3.5 MIAKA MINNE YA RAIS.DKT SAMIA KWA AJILI YA KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

MUUNGANO   MEDIA
0

 






Na Avelina Musa - Dodoma.


KATIKA Kipindi cha Miaka Minne ya Serikali ya awamu ya sita, Mkoa wa Arusha umepokea na kukusanya shilingi Trilioni 3.5, ambazo zimetumika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Mkoa huo.


Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mhe.Kenani Kihongosi leo Julai 20, 2025 Jijini Dodoma wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu mafanikio waliyoyapata katika kipindi cha Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Mhe.Kihongosi amesema miradi ambayo imekamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi walliokuwa na kiu kubwa ya kupata huduma za kijamii zikiwemi za Afya, Maji, Umeme na Barabara kwenye maaeneo yao. 

Amesema Serikali kwa kuzingatia Ilani ya Chama cha Mapinduzi pamoja na Mipango ya Maendeleo ya Kitaifa imeweza  kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, kwa gharama nafuu na kwa wakati.


“Katika Awamu ya Sita Mkoa wa Arusha umepokea na kukusanya fedha kiasi cha shilingi Trilioni 3.5, ambazo zimetumika kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo kwenye sekta mbalimbali,” amesema Kihongosi. 

Amesema mafanikio mengine ni katika sekta ya Afya ambapo Serikali imetoa jumla ya shilingi Bilioni 94.2 kwa ajili ya kuboresha huduma za afya kwa kujenga na kuboresha miundombinu ya afya, ununuzi wa dawa na vifaa tiba.


"Pato la mwananchi katika mkoa limeongezeka kutoka shilingi milioni 3.2 mwaka 2020 hadi shilingi milioni 3.6 mwaka 2023 sawa na ongezeko la asilimia 12.5."Amesema.

Amesema jumla ya shilingi bilioni 958.7 zimetumika kujenga majengo mapya na ya kisasa ya utawala katika Halmashauri za Monduli, Ngorongoro, Arusha Jiji (ujenzi unaendelea) na ujenzi wa ukumbi na nyumba ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa. 


Mkoa wa Arusha ni miongoni mwa Mikoa 31 nchini, wenye Wilaya sita, Halmashauri saba, Tarafa 23, Kata 158, Vijiji 394, Mitaa 154, na Vitongoji 1,505 wenye jumla ya wakazi 2,356,255, kulingana na Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022. 






Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)