Na Avelina Musa - Dodoma.
Wizara ya Madini imeliomba Bunge kuridhia na kupitisha makadirio ya bajeti ya Shilingi Bilioni 224,984,150,000.00 kwa ajili ya matumizi ya Wizara na Taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Aidha,amesema Tanzania imeendelea kuchukua hatua za kuimarisha biashara ya almasi kwa kuanzisha minada, maonesho, masoko na kuhamasisha uwekezaji katika uchakataji wa madini ya almasi ndani ya nchi.
" Mheshimiwa Spika, napenda kulifahamisha Bunge lako Tukufu kwamba Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizobarikiwa kuwa na madini mkakati na madini muhimu (strategic and critical minerals) ambayo yanazidi kuhitajika duniani kwa ajili ya matumizi katika teknolojia za kisasa na nishati mbadala, " Amesema
Hata hivyo ameeleza kuwa mahitaji ya madini haya, yakiwemo lithium, cobalt, nickel, copper, aluminium, zinc, graphite, na rare earth elements (REE), yameendelea kuongezeka kutokana na jitihada za kimataifa za kupunguza hewa ya ukaa ifikapo mwaka 2050 (Net Zero Emission).
Amesema Kuongezeka kwa mahitaji haya kunatokana na kuongezeka kwa uzalishaji wa magari ya umeme, betri za kuhifadhi nishati, na vifaa vya teknolojia ya kisasa vikiwemo simu janja, darubini na kompyuta.
"Mheshimiwa Spika, hali hii inatoa fursa kubwa kwa Tanzania kuhakikisha madini haya yanaongezwa thamani ndani ya nchi ili kuongeza mapato, ajira, na mchango wake katika uchumi wa Taifa," Amesema
Mwisho.