WAZIRI JAFO AKICHJANGIA TAARIFA YA KAMATI YA BUNGE

MUUNGANO   MEDIA
0


Serikali imezielekeza Mamlaka za Serikali za Mitaa kutekeleza jukumu lao la

kuhakikisha taka zote katika maeneo yao zinakusanywa na kutupwa katika

madampo yaliyopo.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na

Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo wakati akichangia taarifa ya utekelezaji ya

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira bungeni jijini Dodoma.

Amesema kuwa kila halmashauri nchini ni lazima iweke utaratibu mzuri wa

zoezi la uzoaji wa taka ngumu na si kuziacha zikizagaa ovyo kwenye mitaa hali

inatoweza kusababisha magonjwa.

“Nashukuru kuna yale madampo matano yaliyojengwa katika mikoa

mbalimbali kupitia mradi lakini baadhi ya halmashauri bado zinasuasua katika

ukusanyaji wa taka..utakuta mtu amepewa tenda (zabuni) halafu hilo lori

lenyewe analotumia ni takataka, hili haliwezekani lazima tufikie mahali

tutumizi majukumu yetu,“ amesema.

Dkt. Jafo ameongeza kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais jukumu lake ni

kusimamia sera wakati halmashauri hizo zinapaswa kutekeleza jukumu lao la

kuhakikisha maeneo yao yanakuwa safi.

Akiendelea kuchangia hoja hiyo, alielekeza kuwa majengo yote yanayojengwa

hasa katika majiji ni lazima yawe na mifumo ya uvunaji wa maji hatua

itakayosaidia kupunguza uharibifu wa miundombinu ya majitaka.

Alisema kuwa miundombinu ya majitaka hasa mifereji inapoharibika

husababisha uchafu kukwama badala ya kwenda kwenye mabwawa ya

majitaka na hivyo kusababisha mafuriko.

Kwa upande mwingine Waziri Dkt. Jafo alisema kuwa mchakati wa uhuishaji

wa Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 namba 191 upo katika hatua nzuri na

unatarajiwa kukamilika mwaka huu.

Alisema kuwa ni kweli sheria hiyo ina mambo mengi yanayotakiwa kuhuishwa

na ni lazima iende na wakati sanjari na Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka

2021 ili ikidhi haja.

Hivyo, Waziri Dkt. Jafo alifafanua kuwa Sheria ya Mazingira inayohuishwa

imegusa mambo mengi ya msingi yakiwemo mchakato wa kulipa nguvu

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kuwa mamlaka

kamili na kukiimarisha Kituo cha Ufuatiliaji wa Kaboni (NCMC).

Awali akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo, Mwenyekiti wake Mhe. Jackson

Kiswaga alisema katika kuhakikisha ukakatiji wa miti unapungua au kuisha


kabisa Bunge linaishauri Serikali kuweka ruzuku katika gesi ili wananchi wawe

na uwezo wa kumudu kutumia nishati hiyo ambayo rafiki kwa mazingira.

Halikadhalika alisema Bunge linaitaka Serikali kuchukua hatua madhubuti

kuhakikisha mchakato wa kuhuisha Sheria ya Mazingira namba 191

unakamilika, ambao unatarajiwa kukamilika mwaka 2024.

Aidha, Mhe. Kiswaga ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kalenga alitoa

ushauri kwa Serikali iweke mwongozo kwa magari yanayobeba taka ngumu

kuyafunika ili zisianguke na kuchafua mazingira.

Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Regina Qwaray aliiomba

Serikali isimamie kanuni na miongozo ya mazingira kukabiliana na wale

wanachafua mazingira.

Pia, Mbunge huyo aliipongeza Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kusimamia vyema

katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki na kuhimizi viwanda viendelee na

shughuli ya urejelejezaji wa chupa za plastiki hatua itakayosadia zisizage ovyo

na kuchafua mazingira.

Alitahadharisha pia kuhusu uchimbaji wa mchanga na kokoto unafanyika

kiholela kwenye makazi ya watu yanatokea na kusababisha makorongo

ambayo hufanya mmomonyoko wa ardhi unaosababisha mafuriko.

 

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)