MIRADI YA UMEME WA JOTOARDHI IENDELEZWE- DKT. BITEKO

MUUNGANO   MEDIA
0



 Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Serikali imeamua

kwa dhati kuendeleza vyanzo vya umeme wa Jotoardhi ili kuhakikisha  nchi inazalisha umeme

wa kutosheleza mahitaji ya wananchi wake.

Amesema chanzo hicho cha umeme kitaongeza nguvu katika vyanzo vilivyopo vya Maji na Gesi

Asilia.

Dkt. Biteko amesema hayo tarehe 20 Februari, 2024 wilayani Rungwe, Mkoa wa Mbeya mara

baada ya kukagua vyanzo vya Jotoardhi vya Kiejo-Mbaka (60MW) na Ngozi (MW 70) mkoani

humo akifuatana na viongozi mbalimbali wa Mkoa wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa, Juma

Homera.

" Miradi hii ya Jotoardhi sasa lazima ianze, tutaanza na megawati 10 hapa Kiejo-Mbaka na

Ngozi tutaanza na megawati 30 huku nyingine zikifuata, na hii inajumuisha miradi mingine

kama wa Jua  wa Kishapu (150 MW) ambao umeanza kutekelezwa, miradi ya umeme wa upepo

ukiwemo wa  Makambako  na mradi wa Malagarasi ambao mkandarasi ameshasaini mkataba

tayari kwa kuanza kazi." Amesema Dkt. Biteko

 Amewaelekeza watendaji wa Kampuni ya Uendelezaji wa Jotoardhi Tanzania  (TGDC) kufanya

kazi zinazoleta matokeo  na si stori kwani Serikali inatafuta fedha za kutekeleza miradi hiyo na

wajibu wa watendaji wa Taasisi hiyo ni kuhakikisha miradi hiyo inafanikiwa.

Dkt. Biteko amesema kuwa,  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu

Hassan anataka kuona watanzania wanapata huduma  bora katika sekta zote,  wanatolewa

kwenye umaskini, anataka vitendo na siyo maneno, anataka kuona watu wahudumiwa na

kufuatwa walipo, wanasikilizwa shida zao na kutatuliwa.

Ameongeza kuwa, Rais, Dkt. Samia anataka utekelezaji wa mipango mbalimbali ya Serikali

iangalie miaka mingi mbele na si muda mfupi hivyo ametoa uhakika kwa wananchi kuwa miradi

hiyo ya Jotoardhi itatekelezwa.

Kuhusu changamoto ya umeme, amesema kuwa, imetokana na vyanzo vya umeme nchini kwa

muda mrefu kujikita  kwenye makundi matatu tu ambayo ni maji (570MW), Mafuta na Gesi 

Asilia.

 Amesema kwa sasa, vyanzo vya umeme vinatokana na Gesi Asilia na Maji ambavyo bado

havitoshelezi mahitaji kutokana na kuzidi kukua kwa maendeleo, idadi ya watu kuzidi

kuongezeka, miji kukua na umeme sasa kuwa ni hitaji muhimu na si anasa.


Amesema  pamoja na kutegemea megawati 235 kutoka mradi wa Julius Nyerere (JNHPP) na

megawati 27 kutoka Rusumo, maboresho ya mitambo mingine ya umeme yanaendelea katika

vituo mbalimbali.

Aidha, ameeleza kuwa, Serikali imeshaamua kutekeleza vyanzo vingine vya umeme ikiwemo

vya Jotoardhi, Jua na Upepo kwani vipo na kinachohitajika ni kuvipa nguvu, 

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amepongeza viongozi wa Mkoa wa Mbeya kwa usimamizi

mzuri wa miradi ya maendeleo pamoja na ushirikiano uliopo kati ya viongozi wa Serikali na

Wabunge wa Mkoa huo.

Awali, Meneja Mkuu wa TGDC, Mhandisi Mathew Mwangomba, amesema  kampuni hiyo ina

miradi mitano ya kipaumbele nchini ambayo ni Kiejo-Mbaka, Ngozi, Songwe, Ruhoi na Natron.

Ameeleza kuwa, kwa Mkoa wa Mbeya miradi ya kipaumbele ni Ngozi na Kiejo-Mbaka ambapo

mradi wa Ngozi unatarajiwa kuzalisha megawati 70 na Kiejo-Mbaka unatarajiwa kuzalisha

megawati 60.

Katika mradi wa Ngozi, amesema kuwa,  utatekelezwa kwa awamu huku awamu ya kwanza

ikitarajiwa kuzalisha megawati 30 na fedha zimeshapatikana ili kuhakiki rasilimali ya Jotoardhi

kwenye eneo hilo.

Ameongeza kuwa, mradi huo wa awali utakaozalisha  megawati 30 utagharimu Dola za

Marekani milioni 144 sawa na shilingi bilioni 369.

Kuhusu mradi wa Kiejo-Mbaka, amesema kuwa, unatarajiwa kuzalisha megawati 60 ambapo

zitaanza kuzalishwa megawati kumi (10) ambazo utekelezaji wake utagharimu Dola za Marekani

milioni 75.64 sawa na shilingi Bilioni 175.88.

Ameongeza kuwa, katika kuhakikisha nishati ya Jotoardhi inapatikana Tanzania, TGDC

imechonga visima vifupi vya mita 300 ambavyo viliwezesha kupatikana kwa temperature

takriban 75 na hii ikithibitisha kwamba kuendelea kuchimbwa kwa visima hivyo kuanzia mita

1500 hadi 1900 itapatikana temperature ya kutosha kuweza kuzalisha umeme.

Vilevile amesema kuwa, nishati ya Jotoardhi ina umuhimu mkubwa nchini kwani ni hakika,

endelevu na salama hasa katika kipindi hiki ambacho dunia inapambana na mabadiliko ya tabia

nchi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera amemhakikishia Naibu Waziri

Mkuu na Waziri wa Nishati kuwa, Mbeya inamuunga mkono Rais, Dkt. Samia katika kulinda

vyanzo vyote ya umeme vinavyogundulika pamoja na utunzaji wa mazingira ambayo

yanapelekea vyanzo hivyo kuzalisha umeme kwa ufanisi.

Pia amempongeza Dkt. Biteko kwa ubunifu wake katika kuendeleza vyanzo vipya vya umeme

ukiwemo wa Jotoardhi.


Caps

moja

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt.Doto Biteko akishuhudia kufunguliwa kwa

valvu  ya kuruhusu majimoto yanayotoka ardhini kupita katika kisima cha utafiti wa Jotoardhi 

katika eneo la Kiejo-Mbaka wilayani Rungwe mkoani Mbeya. Anayefungua valvu ni Meneja

Mkuu wa Kampuni ya Uendelezaji wa Jotoardhi Tanzania ( TGDC), Mhandisi Mathew

Mwangomba.

mbili

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akipanda mti katika eneo

lenyo chanzo cha Jotoardhi, Kiejo-Mbaka wilayani Rungwe mkoani Mbeya ikiwa ni ishara ya

utunzaji wa mazingira ambayo ni muhimu katika uzalishaji wa nishati ya umeme nchini

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)