KAMATI YA BUNGE YAKAGUA MRADI WA KUHIMILI MABADILIKO YA TABIANCHI MPWAPWA

MUUNGANO   MEDIA
0



 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis

Hamza Khamis amewahimiza wasimamizi wa miradi kwenye halmashauri

kuendelea kuisimamia vyema ili ilete tija kwa wananchi.

Amesema hayo wakati wa Ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na

Mazingira ilipotembelea na kukagua Mradi wa Kuhimili Mabadliko ya Tabianchi

kwa kutumia Mifumo Ikoklojia Vijijini (EBARR) katika Halmashauri ya Wilaya ya

Mpwapwa mkoani Dodoma.

Mhe. Khamis amesema kuwa ni muhimu kwa wasimamizi hao kusimamia

vyema fedha zinazoletwa na Serikali kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo, hivyo

kuleta matokeo tarajiwa na kuwanufaisha walengwa.

Pia, amewataka wananchi walionufaika na miradi hiyo kuitunza ili idumu hatua

itakayosaidia kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi zinazoyakabili

meneo kadhaa nchini na duniani kwa ujumla.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya

Maji na Mazingira Mhe. Anna Lupembe ametoa pongezi kwa Ofisi ya Makamu

ya Rais kwa utekelezaji mzuri wa mradi huo.

Mhe. Lupembe ametoa wito kwa wananchi kuzungumzia mazuri yanayofanywa

na Serikali katika kutekeleza miradi hii mikubwa ambayo imewatatulia

changamoto zao.

“Tuipongeze Serikali ya Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan

kwani imewakomboa wananchi kwa kuwatua wanawake ndoo kichwani na

kuwawezesha kujipatia kipato kupitia mradi huu wa maji na kitaku nyumba

tukichotembelea,” amesema.

Miradi ilitembelewa na Kamati ni pamoja na mashine ya kukamua mafuta ya

alizeti na kliniki ya mifugo katika Kijiji cha Ngh’ambi, josho la kuogeshea

mifugo na kisima pamoja na kitaku nyumba katika Kijiji cha Kazania.


Mradi wa EBARR unatekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

(Shinyanga), Mvomero (Morogoro), Mpwapwa (Dodoma), Simanjiro (Manyara)

kwa upande wa Tanzania Bara na kwa upande wa Tanzania Zanzibar

unatekelezwa katika Wilaya ya Kaskazini A, Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Kupitia mradi huu wananchi wanajengewa uwezo wa kuhimili changamoto za

mabadiliko ya tabianchi kwa kuimarisha uwezo wao wa uvumilivu na uwezo

wa mifumo ikolojia inayowazunguka kusaidia katika kuhimili athari za

mabadiliko ya tabianchi.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)