SHULE ZA KIADVENTISTA KIUNGO CHA MAADILI MEMA KWA VIJANA

0

Mch.Gervas Mbipi  Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Mtaa wa Kisasa Jijini Dodoma 


Na.Mwandishi Wetu Dodoma.

Imeelezwa kuwa shule zinazomilikiwa na Kanisa la Waadventista  Wasabato zimekuwa na mchango mkubwa wa kuwalea na kuwajenga watoto katika maadili mema hasa katika ulimwengu huu uliopotea na wenye mmomonyoko wa maadili kwa vijana.


Mch.Gervas Mbipi  Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Mtaa wa Kisasa Jijini Dodoma akiwa katika ibada ya Sabato Kanisa la Waadventista Wasabato Chang'ombe Dodoma.


Hayo yamesemwa na Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Mtaa wa Kisasa Jijini Dodoma Mchungaji Gervas Mbipi katika  ibaada ya Sabato Kanisa la Wasabato Chang’ombe Dodoma iliyokwenda sambamba na changizo maalum kwa ajili ya ukarabati wa Shule ya Iringa Adventist iliyopo Manispaa ya Iringa ambapo makanisa yote ya jimbo la Kati mwa Tanzania(CTF) yamefanya changizo maalum kwa ajili ya shule hiyo.

“Shule za Kanisa  la Waadventista Wasabato zimeanzishwa kwa lengo maalum kuifanya jamii kuwa na maadili mema na kukabiliana na mmomonyoko wa maadili katika jamii ,shule hizi ni kuwaweka sawa vijana kufanya kazi na kutimiza wajibu wao na kuutangaza ufalme wa Yesu Kristo hivyo ni muhimu kuziunga mkono shule  zinawaandaa vijana kuwa jamii bora inayopingana na rushwa,hofu ya Mungu na kuwa taifa bora”amesema.




Baadhi ya Kwaya zikishiriki katika huduma ya Uimbaji Kanisa la Waadventista Wasabato Chang'ombe Dodoma

TAZAMA VIDEO HAPA CHINI


Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)