TUFANYE UTAFITI ZAIDI KUHUSU MAJI DODOMA-AWESO.

MUUNGANO   MEDIA
0

Waziri wa Maji Mhe Jumaa  Aweso (Mb)  ametaka   utafiti ufanyike zaidi  ili kuweza kugundua mabonde mengi yatakayofaa kwa ajili ya uchimbaji wa visima vitakavyoongeza uzalishaji na upatikanaji wa huduma ya maji katika jiji la Dodoma.

Amesema Jiji hilo kwa sasa  uhitaji wa maji ni lita za ujazo mil 133.

Waziri Aweso ameyasema hayo akikagua  mradi wa maji wa Nzuguni ambapo amepokea  mabomba yatakayotumika katika kusambaza maji maeneo ya Nzuguni,Ilazo ,Swaswa na viunga vya jirani,  hadi sasa visima vilivyo chimbwa katika eneo hilo ni visima 5 vyenye uwezo wa kuzalisha lita mil 7 kwa siku.

Mradi  huo ukikamilika utaweza kuwanufaisha zaidi ya  wananchi  75,000.

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)