KILA LA KHERI TAMISEMI QUEENS.

MUUNGANO   MEDIA
0

 


Timu ya mpira wa pete ya ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( OR-TAMISEMI) TAMISEMI Queens  imeagwa rasmi 12 Mei 2023 kuelekea nchini Kenya ambako itashiriki katika mashindano ya Klabu Bingwa  Afrika Mashariki mchezo wa hup yatakayoanza rasmi 13  hadi 20 Mei 2023.


Akizungumza wakati wa kuagana na timu hiyo Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya Ofisi ya Rais -TAMISEMI, Dkt. Charles Mahera  ameitaka timu hiyo kushiriki kikamilifu katika michuano hiyo na kuhakikisha inaibuka kidedea katika michuano hiyo.


"Mnakwenda kwenye mashindano haya na nimeambiwa sio mara yenu ya kwanza kushiriki mwaka jana mlishika nafasi ya nne mwaka huu mkajitahidi kushika nafasi ya kwanza" Amesema Mahera

Mahera amesisitiza kuwa  Ofisi ya Rais-TAMISEMI  itaendelea  kuiongezea nguvu timu hiyo kwakuwa michezo ni  sehemu ya malengo ya kitaifa ya kuhakikisha jamii inandokana na magonjwa mbalimbali hususan magonjwa yasio ya kuambukiza.


Kwa upande wake Kempteni wa timu hiyo Bi. Dafroza  Luhwgo ameihakikishia Ofisi ya Rais-TAMISEMI  kuwa timu hiyo imejifua vilivyo na itahakikisha inaipeperusha vyema bendera ya Tanzania  kwa kuibuka kidedea katika  michuano hiyo.

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)