WATENDAJI KATA WAPOROMOSHEWA PIKIPIKI MBOGWE.

0



Na Makunga Peter  Makunga.

GEITA.

HALMASHAURI ya Mbogwe Mkoa wa Geita imepokea  Pikipiki  6 kati ya 17  na kuwagawia Watendaji Kata ili kuwarahisishia kazi  hasa za ukusanyaji wa mapato.

Habari kamili na Makunga Peter Makunga Kutoka Wilayani Mbogwe.

Hafla hiyo fupi ya kupokea na kuwakabidhi pikipiki watendaji  kata limefanyika katika viwanja vya Halamashauri ya Mbogwe iliyoko kijiji cha kasosobe Bwelwa .

Pikipiki hizo zimetoka kwa Rais Dkt  Samia suluhu hasani kupitia kwa mbunge wa viti maalumu Rose Busiga .

Awali ya yote kaimu mkurugenzi mteji wa halmashauri ya mbogwe  Egidius Kahendaguza  amesema pikipiki hizo zitarahisisha katika shughuli za maendeleo kwa watumishi hao.

Rose Busiga  mbunge viti maalum amewakabidhi pikpiki na kuwaasa wazitunze.


Naye Polisi kata ya Mbogwe  mkaguzi msaidizi  INP DENIS RWEHUMBIZA kwa Niaba ya mkuu wa Polisi wilaya SSP Alex Mkonda  amewataka watendaji kata hao wawe na leseni ya Udereva.

TAZAMA VIDEO HAPA CHINI

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)