WATUMIAJI VYOMBO VYA USAFIRI MKOANI DODOMA WALALAMIKA KUPANDA KWA BEI YA NISHATI YA MAFUTA YA PETROL NA DIZEL.

0

Kufuatia  kupanda kwa bei ya nishati ya mafuta ya petrol,Dizeli na  mafuta ya taa katika soko la dunia kutokana na sababu mbalimbali   zilizotajwa na mamlaka ya udhibiti wa huduma ya nishati na maji [EWURA],baadhi ya watumiaji wa nishati hiyo muhimu  jijini Dodoma wakiwemo madereva na waendesha pikipiki wamelalamikia kupanda kwa mafuta .

 Baadhi ya watumiaji wa vyombo vya usafiri jijini Dodoma akiwemo Athuman Salum pamoja na Khamis Maulid wamesema kupanda kwa mafuta ya petrol na Dizeli imesababisha hali ya uchumi kuyumba .


Aidha,wameiomba serikali kufanya mkakati wan a namna ya kushusha bidhaa hiyo muhimu.

Ikumbukwe kuwa April ,5,2022 mkurugenzi wa Petrol ,kutoka mamlaka ya udhibiti wa huduma ya nishati na maji [EWURA],Gerald Maganga alitangaza ongezeko la bei ya mafuta ya petrol kuanzia April 6,2022 ambapo  bei za rejareja kwa mji  wa Dodoma petrol inanunuliwa kwa Tsh.2920 kwa lita,Dar Es Salaam Tsh.2861 ,Arusha Tsh.2905,huku miji mingine mafuta ya petrol yakiuzwa Zaidi ya Tsh.3000 ikiwemo miji ya Kahama,Kigoma,Mwanza huku chanzo kikitajwa ni mgogoro wa Ukraine na Urusi.


Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)