UKWELI WA MAFUNDISHO YA KIADVENTISTA ,WALETA ROHO 43 KWA YESU KRISTO NA KUBATIZWA KWA MAJI MENGI MALYA KWIMBA.

0




Na.Faustine Gimu Galafoni,Kwimba Mwanza.

Kutokana na ukweli wa mafundisho  ya Biblia yanayotolewa na kanisa la Waadventista Wasabato,jumla ya  watu 43 wamebatizwa kwa maji mengi katika ibaada maalum ya urafiki mwema kanisa la Waadventista Wasabato Malya wilayani Kwimba mkoani Mwanza.

Akizungumza na mtandao huu  mara baada ya kufanyika zoezi la ubatizo  kwa maji mengi ,Mchungaji wa kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa Sumve Wilayani Kwimba mkoani Mwanza  Mch. Zabron Mahega Masanja alisema hiyo ni kutokana na walimwengu kuanza kuelewa mafundisho ya ukweli wa Biblia unaofundishwa na kanisa la Waadventista Wasabato.

“Hivyo,kanisa la Waadventista Wasbato limekuwa  ni kanisa pekee linalotoa mafundisho ya ukweli kuhusu Biblia hivyo kutokana na ukwelli huo watu wamekuwa wakimwamini na kumpokea Yesu Kristo baada ya kupokea mafundisho hayo ,na kutokana na Sabato ya Urafiki mwema jumla ya watu 43 wamebatizwa kwa maji mengi baada ya kuamini na kumpokea Yesu Kristo kama mwokozi wa maisha yao”alifafanua Mch.Mahega

Aidha,Mch.Mahega alitoa wito kwa watu wengine kuendelea kujitokeza na kubatizwa kwa maji mengi kwa makanisa ya Waadventista Wasabato huku akisisitiza kwa Waadventista kuwa nuru kwa kuwaangazia wengine ambao hawajaamini Ukuu wa Yesu Kristo.

Wito tu kwa Waadventista kuwa nuru kuwaangazia wengine kumpokea Yesu Kristo kwa mataifa mbalimbali””alisisitiza.

 

Kwa upande wao baadhi ya watu waliobatizwa kwa maji mengi katika kanisa la Waadventista Wasabato Malya akiwemo Evacate Jefania ,Petro Busiya Joseph ,Naomi Sambay ,Rashid Masasila pamoja na Timotheo Kasuka walisema waliamua kubatizwa kutokana  na kufuatia ukweli wa biblia huku wakiwaasa watu wengine kumfuata Yesu Kristo.

“Kwa kweli mimi nilikuwa wa Imani kutoka dhehebu jingine lakini baada ya kufuatilia ukweli nimeamua kubatizwa  nawasihi wengine kubatizwa kwa maji mengi”alisisitiza mmoja wa waliobatizwa.

Sanjari na hayo Mch.Mahega aliwaasa Washiriki wa Kanisa la Waadventista Wasabato Mtaa wa Malya Wilayani Kwimba Mkoani Mwanza kuendelea  kuwa kielelezo cha  kuwa na mahusiano mema ya kuishi vizuri na jamii inayowazunguka ambapo alisema wanadamu tunategemeana katika nyanja mbalimbali hivyo ni muhimu kuishi katika mahusiano mema.

Aidha,Mchungaji Mahega aliainisha  kanuni za kuishi vizuri na watu kuwa ni pamoja na kudumisha upendo na kuheshimu wengine

Nao baadhi ya wageni waliohudhuria Sabato maalum ya Urafiki mwema akiwemo diwani wa viti maalum  Julieth Mungo pamoja na mwenyekiti wa wafanyakazi shirika la reli Tanzania [TRC]kanda ya Ziwa  Akley Mirambo walielezea jinsi walivyobarikiwa na Sabato hiyo maalum  kuwa ni pamoja na mafundisho mazuri ya Waadventista Wasabato.

“Kwa kweli tunashukuru ukarimu mkubwa tuliofanyiwa na kanisa hili la Waadventista Wasabato Malya kwani hii ndio dini ya kweli kujali watu”alisema Diwani Julieth.

Sabato ya Urafiki mwema katika kanisa la Waadventista Wasabato Malya imekwenda sambamba na utoaji wa  zawadi ya vitabu vya utume vijulikanavyo’’Jipatie amani Moyoni’’ pamoja na uwekaji mikono wakfu kwa  watoto na  pikipiki ya Mchungaji mtaa wa Malya Mch.Kulwa Mbipi iliyotolewa na Jimbo la Nyanza Kusini.

“Kwa kweli nitumie fursa hii kuipongeza Conference ya Nyanza kusini kwa kutujali kununua usafiri wa pikipiki hii maana eneo la Malya jiografia yake maeneo yako mbalimbali  na wakati mwingine tulitembea kwa miguu au kuazima baiskeli na waumini walinishika mkono kweli wengine waliniazimisha pikipiki,hivyo ununuzi wa pikipiki hii yenye Zaidi ya Tsh.Milioni mbili itasaidia sana kutembelea maeneo mengi Zaidi kupeleka injili”alisema Mch.Mbipi.

 

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)