Mwonekano kwa mbele shule ya Msingi Mwanhegele Wilayani Maswa Mkoani Simiyu.
Moja ya kombe lililotolewa na serikali kwa shule ya Msingi Mwanhegele kutokana na shule hiyo kuendelea kufanya vizuri mitihani ya Taifa.
Mmoja wa walimu katika shule ya msingi Mwanhegele akitekeleza majukumu yake ya ufundishaji
Mazao ya chakula yanayotumika katika kipindi cha makambi ya masomo.
Na.Faustine
Gimu Galafoni,Maswa Simiyu.
Shule ya
Msingi Mwanhegele iliyopo Wilayani Maswa Mkoani Simiyu ambayo imekuwa ikishika
kumi bora kwa miaka 6 mfululizo katika shule za serikali Tanzania huku matokeo ya mwaka jana ikishika nafasi ya
Kwanza kwa shule za serikali ambapo changamoto zinazoikabili shule hii
ikiwemo kukumbwa na wanyama wakali kama vile fisi na ukosefu wa umeme zimegeuzwa kama fursa.
Mwalimu mkuu wa shule ya Msingi
Mwanhegele ,Mashala Kija akifanya mahojiano maalum na Mtandao huu mwanzoni mwa Juma lililopita alisema moja ya juhudi wanazozifanya ni kuanzisha
makambi ya kujisomea nyakati zote za usiku na
mchana kwa madarasa
yanayokabiliwa na mitihani ya kitaifa ambapo mwaka jana palitokea
changamoto ya kuvamiwa na wanyama wakali
wakiwemo fisi lakini
walishirikiana na wananchi kuwasaka fisi na kuendelea kujisomea nyakati za
usiku.
“Shule hii imefanya jitihada
mbalimbali ambapo mwaka jana imekuwa ya Kwanza Tanzania,changamoto kubwa
zinazoikabili shule hii mfano,wakati tukiwa makambi tulianza kuvamiwa na fisi
katika maeneo haya lakini tuliweza kupambana kwa kushirikiana na wananchi
,hatukurudi nyuma maana nyakati za usiku wanafunzi wakiwa wajisomea fisi
walikuwa wanakuja hii ni kutokana na jiogerafia ya maeneo haya”alisema mwalimu Mashala.
Aidha,Mwalimu
mkuu huyo alisema changamoto ya kutokuwa na miundombinu ya umeme shuleni hapo
imewapa fursa ya kununua umeme jua[sola]kwa ajili ya kuruhusu wanafunzi
kujisomea nyakati za usiku
“Licha ya shule hii kufanya vizuri
tunakabiliwa na changamoto ya kutokuwa na umeme ,na umeme tunaotumia hadi sasa
ni umeme wa jua hii ni kutokana na wazazi kushirikiana kwa kufanya michango na
kufanikisha kununua umeme jua[sola] lakini mkakati wa serikali ni kutandaza
umeme wa TANESCO kwa mujibu wao walisema umeme huo unaweza kuwasha kuanzia
mwezi wanne”alisema.
Mwalimu
Mashala aliainisha Changamoto nyingine ni utokuwa na miundombinu ya nyumba za
walimu hata moja hali ambayo huwalazimu walimu kupanga wilaya jirani ya Kwimba
mkoani Mwanza.
“Kwa kweli hii ni changamoto kubwa
kwani walimu wanapanga wilaya jirani ya
Kwimba mkoani Mwanza ,na wanapofundisha usiku wakimaliza inabidi wasubiriane
kwenda nyumbani nyakati za usiku kwani ni mbali kidogo hilo ndio ombi letu kubwa kwa serikali
itusaidie angalau hata nyumba mbili za kuanzia maana hakuna hata nyumba moja ya
mwalimu”alifafanua
Mwalimu Mashala.
Mwenyekti wa
Kamati ya Shule ya Msingi Mwanhegele ,Mathias Gabriel alisema ushirikiano kati
ya kamati ya shule na walimu ndio nguzo muhimu inayosaidia kufaulisha wanafunzi
.
“Sisi kama kamati ya Shule tuna ushirikiano
mkubwa na walimu na tunawaheshimu sana kutokana na kazi ngumu wanazofanya na
huwa tunajitahidi kuwatia moyo”alisema .
Baadhi ya
walimu katika shule hiyo walisema umoja na ushirikiano ndio nguzo muhimu inavyochochea kiwango cha
ufaulu katika shule hiyo.
“moja ya mkakati tunaofanya ni
kuhakikisha mtoto apandi darasa kama hajui kusoma ,kuandika na kuhesabu hivyo
ushirikiano wetu pamoja na uongozi na kamati ya elimu umekuwa nguzo muhimu na
tunahakikisha tunakuwa lugha moja”alisema mmoja wa walimu hao.
Kwa upande
wao baadhi ya wanafunzi darasa la saba shule ya Msingi Mwanhegele akiwemo
Agnes Paul Cosmas pamoja Elia
Andrea waliahidi kufanya vizuri kwa
mwaka huu kama walivyofanya watangulizi wao.
Katika
utatuzi wa changamoto za ukosefu wa miundombinu shuleni hapo,Afisa Elimu,Wilaya
ya Maswa Lucy Kulong’wa alisema serikali ina mpango wa ujenzi wa nyumba za
walimu katika shule mbalimbali wilayani Maswa.
Ikumbukwe
kuwa shule ya msingi Mwanhegele Maswa Simiyu imekuwa ya kwanza kwa shule za serikali katika matokeo ya
mtihani kumaliza elimu ya Msingi Tanzania
zikifuatiwa na shule ya Msingi Kagera ,shule ya msingi Stesheni
Lindi,shule ya msingi Butimba B,Butimba ,Majengo mkoani Lindi ,Mnarani Mkoani
Mwanza ,Kisimani Mkoani Arusha,Nyasa mkoani Mbeya na nafasi ya kumi ilikuwa ni
shule ya Msingi Mianzini kutoka mkoani Lindi.
MWISHO.