RC MTAKA AWATAKA WATUMISHI HALMASHAURI YA CHEMBA WAJITAFAKARI KATIKA UTUMISHI WAO

1


TAZAMA VIDEO HAPA CHINI


 



Na.Faustine Gimu Galafoni,Chemba Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka amewataka watumishi wa halmashauri ya Chemba kujitafakari  katika utumishi wao  kutokana na halmashuri hiyo kurudi nyuma kimaendeleo    kwa kudorora ukusanyaji wa mapato,kiwango cha chini  ufaulu na miradi mbalimbali kutotekelezwa kwa wakati, chanzo kikitajwa kuwa ni malumbano na mivutano isiyo na tija kwa watumishi wa halmashauri hiyo.

Mkuu wa Mkoa huyo amebainisha hayo  Wilayani Chemba Mkoani Dodoma baada ya kufanya mkutano  na Watumishi  wa halmashauri hiyo ngazi ya vijiji hadi wilaya lengo ni kusikiliza kero pamoja na changamoto mbalimbali zinazosababisha halmashuri  hiyo kusuasua katika nyanja mbalimbali zikiwemo nyanja za elimu,Kilimo ,na miradi mbalimbali ya maendeleo kukwama  kutokana na  malumbano kwa viongozi  wanavyoeleza.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Said Sambala ,diwani wa kata Jangalo Abdu Msuri ,diwani wa kata ya  mrijo Abdallah Satti pamoja na mjumbe kamati ya fedha Mwanahamis Batu wamesema malumbano ya kila siku imekuwa changamoto katika halmashauri hiyo.


Mbunge wa jimbo la Chemba Mohammed Moni naye amekiri kuwa baadhi ya watumishi wa halmashauri hiyo wamekuwa vikwazo kwani wamekuwa wakipuuza   hata ushauri  unaotolewa .


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka amemtaka mkurugenzi wa halmashauri hiyo kuwa  makini na ushauri wa upotoshaji anaopewa na  baadhi ya watumishi wake hususan wakuu wa idara.


Hivyo,Mkuu huyo wa mkoa amewataka watumishi wa halmashauri ya Chemba kujitafakari  kwani halmashauri haiwezi kuendeshwa kwa malumbano.

Katika kuhakikisha Wilaya ya Chemba inasonga mbele kimaendeleo ,amewataka viongozi kuibua miradi kwa kuangalia mashamba kwa vijiji   na shule zenye wazalishaji wakubwa wa mazao ili aweze kufanya ziara  na kuweka mikakati imara ya  namna ya kuvisaidia vijiji  na  maeneo hayo kukuza uzalishaji.


Kuhusu suala la watendaji wa vijiji na kata  kubambikiziwa madeni kutokana na hitilafu ya mifumo ya mashine ya kukusanyia mapato kuwa na changamoto ya kujirudiarudia utoaji wa stakabadhi mkuu huyo wa mkoa ameagiza wafutiwe madeni mara moja kwani hiyo ni kuwakatisha tamaa huku akikitaka kitengo cha TEHAMA kufanya uhakiki wa mashine hizo na kubaini kasoro zilizojitokeza.

Kuhusu suala la Elimu  wilayani Chemba ,Mkuu huyo wa mkoa amesema haiwezekani shule iwe na wanafunzi 13 halafu  baadhi yao wafeli mtihani hivyo ni vyema wadau wa elimu Chemba kuja na ubunifu katika kuhakikisha kiwango cha elimu kinaongezeka .

MWISHO.

Tags

Chapisha Maoni

1Maoni
Chapisha Maoni