WAZAZI WASHIRIKI UTOAJI WA MIMBA LUNGUYA MSALALA KAHAMA

0



 Na.Faustine Gimu Galafoni.

Imeelezwa kuwa kuna  changamoto ya baadhi ya wazazi na walezi  kata ya Lunguya halmashauri ya Msalala kushiriki kutoa ujauzito kwa mabinti zao suala ambalo ni hatari kwa afya .

Hayo yamejiri katika ziara ya mbunge wa jimbo la Msalala wilayani Kahama Ezekiel Maige katika kijiji cha Madaho kata ya Lunguya wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.
Mmoja wa  wananchi wa kijiji hicho Kazimili Pascal  amesema kuwa tatizo la utoaji wa ujauzito kwa wasichana limekuwa likisababishwa na baadhi ya wazazi.


Akijibu hoja hiyo mbunge wa jimbo la Msalala amesema kuwa suala la utoaji mimba ni kosa la jinai hivyo amewaomba wananchi kuwa na  ushirikiano  kwa kutoa taarifa dhidi ya watu wanaojihusisha na utoaji wa mimba.

Aidha Maige amewaasa vijana kuepuka kuwashawishi  watoto wa kike kujihusisha na Mapenzi.

Ziara ya Maige inaendelea leo katika jimbo la Msalala   yenye lengo la kujionea shughuli mbalimbali za Maendelio

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)