MACHINGA WA HOSPITALINI WAANDAMANA KAHAMA

0


 Na.Faustine Gimu ,Kahama.
 
Wafanya biashara ndongondogo Maarufu kama Wamachinga  katika  eneo la hospitali ya mji wa Kahama wameandamana hadi  Katika ofisi za chama cha mapinduzi CCM   kupinga agizo la mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya mji wa Kahama la kuwahamisha katika eneo hilo.

Tukio hilo limetokea Jana  majira ya saa tano  asubuhi jambo lililopelekea uongozi wa CCM  kufanya kikao cha dharura na mkuu wa wilaya ya Kahama na mkurungenzi mtendaji wa halmashauri hiyo.
Wakizungumza na waandishi wa habari ,baadhi ya wafanya biashara  hao Saimon Nsabile  na  Joshua Wiliam wamesema kuwa  wamehamishwa bila kufuata utaratibu.

Madai yao yametupiliwa mbali na mkurugenzi  mtendaji wa halmshauri hiyo Underson Msumba ambapo amesema eneo lao wametengewa katika eneo la CDT na hakuna machinga anayeruhusiwa kufanya biashara eneo hilo.

Hata hivyo wafanyabiashara hao wamepinga suala hilo wakidai kuwa eneo wanakopelekwa haliendani na bidhaa wanazouza.
Kwa upande wake  diwani wa kata ya Kahama mjini Hamidu Juma Kapama amesema kuwa jambo hilo ni mpango wa Mkurugenzi  na halijapitishwa na baraza la madiwani.

Na.Faustine Gimu.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)