WANANCHI MWASHIGINI MSALALA KAHAMA WACHANGIA ZAIDI YA TSH.MILIONI 3 KWA UJENZI WA ZAHANATI

0


Wananchi wa kijiji cha Mwashigini kata ya Mwakata halmashauri ya Msalala wilayani Kahama Mkoani Shinyanga wamechangia zaidi ya shilingi milioni tatu kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho.

Hayo yamesemwa na diwani wa kata ya Mwakata Ibrahim Six Masanja wakati akizungumza na Gimu Blog.

Masanja amesema kuwa katika mchango huo kila kaya imechanga kwa shilingi elfu 10 huku mfuko wa jimbo kupitia kwa  mbunge wa jimbo la  Msalala Ezekiel Maige umechangia Zahanati hiyo.

Hata hivyo Diwani huyo amesema kuwa kazi ya ujenzi wa zahanati unaendelea baada ya maji ya ujenzi kupatikana katika kipindi hiki cha masika .

Sanjari na hayo Masanja amesema kuwa kuna zaidi ya bati  2000 na tofali 30 elfu katika kata yake zilizotokana na msaada wa maafa ya mvua ya barafu  Mwakata.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)