WANUFAIKA TASAF KAHAMA WAONYWA KUTOBWETEKA NA PESA NA BADALA YAKE WALIME

0
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Bi.Zainabu Rajab Terack amewatakata waratibu wa TASAF Wilayani Kahama kuwahamasisha walengwa wa TASAF  kuacha kubweteka na badala yake wajikite katika kilimo.

Hayo ameyasema  katika ziara yake Mjini  Kahama yenye lengo la kuhimiza wananchi  kujikita katika kilimo  na kuacha utegemezi.
Mkuu huyo wa mkoa amesema kuwa msimu wa kilimo bado unaendelea ambapo amezitaka kaya masikini kulima na walengwa wa TASAF  watakaokaidi   agizo watakosa fedha za TASAF.

Afisa  ushauri na ufuatiliaji wa TASAF   katika halmashauri za mji wa Kahama na Ushetu   Prospa Malengo amesema kuwa wamepokea maagizo na maelekezo hayo na kuongeza kuwa watayafanyia kazi.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)