MTOTO ALIYEPOTEA KAHAMA FUVU LAPATIKANA

0


Baadhi ya viungo vya mwili ikiwemo kichwa pamoja na nguo vinavyodhaniwa kuwa ni vya Mtoto  Teresia Dickson  mwenye umri wa  miaka 3 mkazi wa kijiji cha Namatutu kata ya Bulungwa halmashauri ya Ushetu  Mkoani Shinyanga,vimepatikana   katika kijiji cha Busulwanguku kata ya Idahinha.

Akizungumza na Baloha FM redio baba mzazi wa mtoto huyo Dickson Paul amesema kuwa  mtoto huyo alipotea tangu Januari 22 mwaka huu baada ya kwenda kucheza na watoto wenzake lakini hakulejea ndipo walipoanza harakati za kumtafuta.

Mwenyekiti wa kijiji cha Namatutu Simon Mwendwa ameelezea juu ya kupata taarifa hizo ambapo amewataka wanachi kuwa makini kuwalinda watoto wao.

Naye Afisa mtendaji  wa kijiji  William Msoselo amezungumzia juu ya kupokea taarifa za kupotea mtoto huyo  ndipo jitihada za kumtafuta mtoto huyo zikaanza ndipo walipoona fuvu na nguo alizokuwa amevaa.

Nao baadhi ya wananchi mashuhuda wa tukio hilo wamesikitishwa kutokea

kwa tukio hilo huku wakiitaka serikali kuendelea kuimarisha ulinzi na usalama.

Kamanda wa polisi mkoani Shinyanga Simon Haule ameelezea kupata taarifa hizo na kuahidi kufuatilia ambapo uchunguzi zaidi unaendelea ili kujua  chanzo cha tukio hilo.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)