TERACK AAGIZA BUZWAGI KUJENGA NYUMBA YA SAKALI UWANJA WA NDEGE

0


Mkuu wa mkoa wa SHINYANGA ZAINAB TELACK amewaagiza ACACIA kuhakikisha wanatengeneza sehemu ya makazi ya Askari ndani ya eneo la uwanja wa ndege.

Ametoa agizo hilo  katika  makabidhiano ya uwanja huo wakati ukaguzi wa eneo hilo  ukiendelea  ambapo amesema askari wanatakiwa kukaa sehemu nzuri ili waweze kufanya kazi vizuri hivyo pamoja na kukabidhi wanatakiwa kutengeneza ili iwe sehemu ya kudumu.

Kwa upande wake Meneja mkuu wa mgodi wa Buzwagi BENADICT BUSUNZU amesema watalifanyia kazi jambo hilo ili kuhakikisha wanaboresha na kutoa mchango kwa vitu ambavyo vitahitajika katika uwanja huo.

Hata hivyo BUSUNZU amesema pamoja na kukabidhi uwanja huo wataendelea kushirikiana na serikali katika mambo mabalimbali ya kimaendeleo ili kuibua huduma ambazo zitachochea mendeleo.



Uwanja wa huo wa ndege uliopo katika eneo la BUZWAGI Mwendakulima wilayani Kahama ulikuwa chini ya Mgodi  Wa ACACIA ambapo  Januari 25 mwaka huu  Umekabidhiwa rasmi mikononi mwa serikali chini ya Naibu waziri wa Ujenzi ELIAS KWANDIKWA. 

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)