Naibu
waziri wa ujenzi Elias Kwandikwa
amewahakikishia wananchi wa kata ya Ulewe halmashauri ya Ushetu mkoani Shinyanga kuimarisha miundombinu ya
barabara ambayo imekuwa changamoto katika kata hiyo ikiwa ni pamoja na
ukarabati wa Daraja la Ilangashika.
Akizungumza
na wananchi wa kata Ulewe katika eneo ya daraja hilo ambalo limekuwa
kikwazo kikubwa cha maendeleo Kwandikwa
amesema kuwa baada ya kukamilisha maeneo yaliyo kuwa na changamoto kubwa
yakiwemo madaraja ya Kalo,Kasheshe na
Kidanha ambayo yamegharimu pesa nyingi sasa ni wakati
wa kushughulikia miundombinu ya Ilangashika.
Kwa upande
wake diwani wa kata ya Ulewe Kulwa Emmanuel
ameiambia Baloha FM kuwa ujio wa Naibu waziri huyo wa ujenzi ni faraja kwa wananchi ambapo
amebainisha kuwa daraja hilo linamekuwa adha kubwa kwani limekuwa likisababisha
magari mengi kuharibika na nauli kuwa ghali.
Katika
hatua nyingine Naibu waziri wa Ujenzi Elias Kwandikwa amesema kuwa kukamilika kwa barabara ya mkato
ya Mseki Bulungwa itarahisisha kufika
makao makuu ya Halmashauri ya Ushetu kwa haraka zaidi hivyo itafungua wigo wa uchumi endapo itapanuliwa na kukarabatiwa.
Kwandikwa
tangu ateuliwe kuwa
Naibu waziri wa ujenzi Mwaka huu ,ameshabakiza kufanya ziara mikoa 7
pekee ili kuieneza Tanzania nzima ambapo
leo anaendelea na ziara katika halmashauri ya Ushetu mkoani Shinyanga kwa lengo
la kujionea miundombinu ya barabara na kufanya tathmini ya gharama za ujenzi
akiwa na watalaam kutoka Mamlaka ya
barabara mjini na vijijini TARURA na TANROADS.