MWENYEKITI WA BUSINDI MSALALA KAHAMA ALALAMIKIWA KWA KUONGOZA KIMABAVU

0


 MWENYEKITI WA BUSINDI MSALALA KAHAMA ALALAMIKIWA KWA KUONGOZA KIBABE.

 MBUNGE WA MSALALA EZEKIEL MAIGE

Wananchi wa kijiji cha Busindi  kata ya Bulyanhulu halimashauri ya Msalala Wilayani Kahama, wamelamikia kitendo cha Mwenyekiti wa kijiji hicho MUYA DOMINICK kushindwa kusoma mapato na matumizi na kuwaongoza kwa mabavu.

Hayo yameibuka katika ziara ya Mbunge wa jimbo hilo Ezekiel Maige wakati akifanya mkutano wa hadhara na wananchi hao kijijini hapo.

Mmoja wa wananchi wa eneo hilo  FRANCISCO TUMBOWANANE akitoa kero zinazowakabili amesema kiongozi huyo amekuwa kero kwa wananchi kwa kuwa hajawahi kusomewa mapato na matumizi tangu mwaka 2016.

Diwani wa viti maalumu PRISCA MSOMA ameshiriki katika mkutano huo na kusikiliza kero nyingi zikiwasilishwa kwa Mbunge huku anasikitishwa na kinachoendelea kijijini hapo kwakuwa amesikia wananchi wakilalamikia pia suala la kiongozi huyo kutoa nafasi za ajira zinapotokea kwa upendeleo kwa wafuasi wa chama chake cha CHADEMA pekee.

Mwenyekiti huyo anayetupiwa lawama akijibu hoja zilizoibuliwa na wananchi amekiri kutoa upendeleo wa ajira zinapojitokeza na kuwapa wanachama wa cha  CHADEMA kwakuwa ni wafuasi wa chama chake huku akisema amekuwa akishindwa kusoma mapato na matumizi kwakuwa nyaraka zimepotea.

Kufuatia sakata hilo Mbunge wa Jimbo la Msalala Ezekiel Maige amemwagiza diwani wa Kata hiyo John Kiganga kulifuatilia.

Ziara ya Mbunge huyo inaendelea tena kesho katika maeneo mengine ya jimbo hilo ikiwemo Kijiji cha Sungamile.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)