VIFAA VYA SHULE VYAPANDA KAHAMA KATIKA MSIMU HUU WA KUFUNGUA SHULE

0


Ikiwa kesho shule mbalimbali  hapa nchini zinatarajia kuanza masomo baada ya likizo  baadhi ya vifaa vya shule mjini Kahama vimepanda bei kutokana na uhitaji kuwa mkubwa kwa wanafunzi  ikilinganishwa na hapo nyuma.
Hayo yamesemwa leo na baadhi ya wateja wa mahitaji ya vifaa vya shule ambao ni wazazi wa wanafunzi walipokuwa  katika manunuzi  soko la  uwanja wa taifa eneo la  Majengo mjini Kahama.

Wazazi hao wamesema kuwa wafanyabiashara wamepandisha bei  kwa bidhaa za shule baada ya kuona kuna wateja wengi huku wakiwaasa watoto wao kusoma kwa bidii katika kipindi hiki kigumu kwani elimu ni ufunguo wa maisha.

Kwa upande wao baadhi ya wafanyabiashara wa vifaa vya shule ikiwemo viatu na nguo wamesema kuwa biashara imekuwa nzuri kwao na sababu ya kupandisha bei ni kutokana na uhitaji mkubwa.

Naye mmoja wa wanafunzi  ameahidi wazazi kusoma  kwa bidii  kwani wazazi wake wamekuwa wasaidizi wakubwa katika masuala yake ya shule.

Shule mbalimbali za msingi na sekondari hapa nchini zinatarajia kufunguliwa kesho Januari 8 ,tayari kwa kuanza muhula mpya wa Masomo 2018 na wanafunzi kupanda ngazi mbalimbali za madarasa na vidato.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)