KONGAMANO LA MWANADALO 2018=WANAOUA ALBINO NA VIKONGWE WAKAMATWE

0


Jamii wilayani Kahama mkoani Shinyanga imeaswa kudumisha mila na desturi  za kitanzania kwa kupinga mauaji ya vikongwe na  watu wenye ualbino.

Hayo yamesemwa na mtemi wa Sungusungu wilayani Kahama mkoani Shinyanga Machimu Mwanandalo katika kilele cha kongamano la Mwanandalo la kudumisha mila na desturi lililofanyika  kata ya Mwakata Halmashauri ya Msalala.
Mwanandalo amesema kuwa ni vyema jamii ikawa na uelewa juu ya vitendo viovu ambavyo  vimekuwa vikiwadhalilisha waganga havina budi kupingwa vikali na serikali.

Nao baadhi ya wanachi waliohudhuria akiwemo diwani wa kata ya Mwasala Mkoani Tabora wamezungumzia juu ya kongamano hilo.

Kitikiti Masai ni mwakili wa Sadick Kisenga  ambapo ameelezea juu ya zawadi hiyo ambayo amekabidhiwa mwenyekiti  wa Sungusungu Wilaya ya Kahama Machimu Mwanandalo..

 Kongamano la mila na desturi la Mwanandalo 2018 limeenda sambamba na upokeaji wa zawadi ya trekta moja aina ya  S.H lenye thamani ya  Sh.milioni 20 na   gari Landcruiser moja lenye thamani ya shilingi milioni 40 yote yametolewa na  Mfanyabiashara maarufu kutoka mkoani Morogoro Sadick Kisenga  baada ya kufurahishwa na kongamano hilo

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)