CCM NYASUBI YATOA MSAADA KTUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA MUVUMA

0



 Image result for nembo ya ccm tanzania

Katika kuelekea  kuadhimisha kilele cha kutimiza miaka 41 ya chama cha mapinduzi  CCM  tangu kuanzishwa  kwake mwaka 1977,chama cha mapinduzi kata ya Nyasubi wilayani Kahama Mkoani Shinyanga  kimetembelea kituo cha kulelea watoto wanaoishi mazingira hatarishi Cha MUVUMA Nyasubi  na kutoa msaada wa vitu mbalimbali.

Akizungumza katika eneo la kituo hicho,Katibu wa CCM kata ya Nyasubi Mlawa Nyili amesema kuwa Lengo la kufika kituoni hapo ni kuwafariji watoto na kujionea changamoto zao huku akitaja baadhi ya msaada wa vitu walivyotoa.

Mwenyekiti wa CCM kata ya Nyasubi Bathelomeyo Kayoka  ameitaka jamii Wilayani Kahama  kuwa na tabia ya kusaidia watoto waishio katika mazingira hatarishi na kuacha tabia ya unyanyapaa kwani nao ni binadamu kama  watu wengine.

Walezi wa kituo hicho Anatulia Petro na Eliya Mpenda wameomba jamii nyingine iwe na moyo  kama huo huku wakikiomba chama cha mapinduzi CCM kuendelea kutoa misaada .

Kwa upande wao watoto wanaolelewa katika kituo cha MUVUMA wamekipongeza chama cha mapinduzi CCM kwa kutoa msaada huo.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)