IDARA YA DORIKAS KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO MALUNGA YATOA MSAADA MAGEREZANI

0
Idara ya wanawake ya Dorikas Kanisa la waadventista wasabato Malunga wilayani Kahama mkoani  Shinyanga  imetoa msaada wa vitu mbalimbali  kwa wafungwa katika gereza la Kahama vyenye thamani ya Zaidi ya Sh.Laki 3.

Akizungumza na   GIMU BLOG  mara baada ya kumalizika utoaji wa msaada  huo,mkuu wa Idara ya Dorikas Kanisa la waadventista wasabato Malunga  mjini Kahama Veronica Lameck amesema kuwa vitu vilivyotolewa ni nguo ,sabuni ,mafuta  na miswaki vyenye thamani ya shilingi laki 3 na 85 elfu na 100.

.
Mzee wa kanisa la waadventista wasabato Malunga Manase Alphonce ametoa wito kwa waumini na viongozi kutoka taasisi mbalimbali kuwa  na moyo wa kuendelea kutoa misaada kwa wahitaji.

Naye mmoja wa waumini wa kanisa la waadventista wasabato Malunga Christina Lukwalo amesema kuwa ni wajibu wa kila mtu kuwasaidia  watu wenye uhitaji maalum ikiwa ni pamoja na wafungwa,wajane,yatima na wazee na kuacha tabia ya kuwanyanyapaa na kuwatenga.

Kwa upande wake Kaimu mkuu ambaye pia ni  mrakibu  wa gereza la wilaya ya Kahama Lusana Shigumha amelipongeza kanisa hilo kwa kuwajali wafungwa huku akizitaka taasisi zingine kufanya hivyo.


Utoaji wa wa misaada kwa watu wenye uhitaji maalum ni moja ya kipaumbele kikuu  kinachofanywa  na kanisa la waadventista wasabato ulimwenguni pote kama maagizo  ya yesu kristo yasemavyo kuwasaidia wafungwa ni jambo la  busara.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)