DC NKURLU AWAPA POLE KAHAMA KWA KUKOSA MAJI

0


Mkuu wa wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga Fadhil Nkurlu amewapa pole wananchi wa kahama kwa tatizo la maji lililo kuwepo kwa zaidi ya wiki moja

Mkuu huyo wa wilaya amesema kuwa tatizo hilo limekuwa likijitokeza kutokana na mamlaka ya maji ya mjini shinyanga kashuwasa kwa kukatiwa huduma ya umeme kutokana na deni wanalodaiwa na shirika la umeme na hivyo kuathiri upatikanaji wa maji.

Aidha amesema kutokana na hali hiyo leo ameketi na bodi ya maji ya kuwasa ili kuweza kutafuta ufumbuzi wa kudumu ili tatizo hilo lisijirudie tena kwani limekuwa likisababisha watu kukosa maji safi na salama.

Katika hatua nyingine Nkurlu amewapongeza wazazi waliojitokeza kuwaandikisha elimu ya msingi,pamoja na kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi wanaojiunga na kidato cha kwanza.
Amesema kumekuwa na jitihada binafsi anazozifanya baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na muwakilishi mkazi wa umoja wa mataifa nchini na kumuomba kutatua changamoto mbali mbali ikiwemo katika sekta ya elimu.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)