Mbunge wa Jimbo la chemba Mhe. Kunti Majala amefanya mkutano wa hadhara wenye lengo la kusikiliza kero za Wananchi katika kata ya Gwandi na kutoa Ufafanuzi wa Changamoto zilizowasilishwa ya miundombinu ya barabara,mawasiliano pamoja na Migogoro ya ardhi.
Mhe. Kunti amefanya mikutano hiyo katika vijiji 3 na kitongoji 1 vinavyounda kata ya Gwandi ambapo imefanyika katika Kijiji Cha Muungano huku akitoa vifaa vya michezo jezi na mpira.
Aidha katika Kijiji Cha Rofati, Mhe.Kunti ametoa vifaa vya michezo jezi na mpira
na katika kijiji Cha gwandi, alitoa vifaa vya michezo jezi na mpira pamoja na kitongoji Cha Toroma.
Hata hivyo wananchi wa kata ya Gwandi wamemshukuru na kumpongeza Mhe. Kunti Majala kwa kutatua kero zao pamoja na kumkabidhi zawadi mbali mbali.




