VIONGOZI WOTE TABORA WAAGIZWA KUTEKELEZA MPANGO JUMUISHI WA WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII.

MUUNGANO   MEDIA
0

 

 

Mhe. Paul Matiko Chacha Mkuu wa Mkoa wa Tabora.

.

Na. Elimu ya Afya kwa Umma.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora,Mhe. Paul Matiko Chacha amewaelekeza viongozi wote ngazi ya Mkoa na Halmashauri kuhakikisha kuwa wanatekeleza mpango Jumuishi wa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii kwa mujibu wa Miongozo ya Serikali.

Mhe. Chacha ametoa maelekezo hayo Juni 10,2024 wakati amefungua Kikao cha kujadili Utekelezaji wa Mpango Jumuishi wa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii Mkoani Tabora.



Aidha, ametoa shukrani kwa Wadau wote wanaoendelea kushirikiana na Serikali ya awamu ya Sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuboresha huduma za afya nchini.

Halikadhalika, amesisitiza kuwa kuwa katika Mkoa wa Tabora Serikali inaendekea kufanya mambo mengi katika sekta ya afya ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa mpango huu utaokuwa na manufaa makubwa kwa wananchi wa Tabora huku akiipongeza Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kuweka Mkoa wa Tabora miongoni mwa mikoa ya kipaumbele.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa huo Dkt. John Mboya amewahimiza Viongozi na wajumbe wote kuepuka vitendo vyote kinyume na mwongozo katika ngazi zote.Dkt. John Mboya,Katibu Tawala wa Mkoa huo.

 

Wajumbe wa kikao hiki ni Viongozi mablimbali wa Mkoa na Halmashauri zote nane (8) wakiweno Wakuu wa Wikaya na Wakurugenzi.

 

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)