SERIKALI INATAMBUA UMUHIMU WA DINI NA TAASISI ZA KIDINI RC -SENYAMULE

MUUNGANO   MEDIA
0


 

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ametoa tamko hilo leo Februari 05, 2024

alipofanya ufuatiliaji wa Taasisi ya Ally-Habshi inayojishughulisha kutoa mafundisho ya Madrasa kufuatia

kukamatwa kwa Mwalimu wake Bw. Yusuph Mohamed kwa tuhuma za kukutwa akitoa mafundisho ya

Dini kwa watoto 132 kwenye mazingira hatarishi yasiyo na huduma muhimu za Kijamii.


Akizungumza na waandishi wa Habari wakati alipotembelea kituo cha kulelea watoto wenye uhitaji

kilichopo Kata ya Kikombo Jijini Dodoma ambacho ndicho watoto hao walipelekwa baada ya kutolewa

kwenye maeneo waliyokutwa Mtaa wa Sogeambele na Nkuhungu kufuatia kukamatwa kwa Mwalimu

wao.


Mhe. Senyamule amesema Serikali inatambua umuhimu wa Dini,Taasisi za Dini na nafasi ya viongozi wa

Dini zote katika kujenga kizazi chenye hofu ya Mungu na kuwa na maadili mema.


Hata hivyo, ameongeza kuwa Mafunzo ya Dini kwa watoto ni jambo lenye umuhimu mkubwa na

linaugwa mkono na Serikali kwani Mkoa unashirikiana kwa Karibu na viongozi wa dini katika mikakati

mbali mbali ya maendeleo ya Mkoa.


“Taasisi ni lazima kabla ya kuanzishwa, ifuate vigezo vyote vinavyotakiwa vya kijamii, naelekeza usajili na

uendeshaji wa makao ya watoto ufuate utaratibu.


“Taarifa ya awali ya ukaguzi wa miundombunu ya Taasisi hii imebainisha ukiukwaji wa sheria. Viongozi

wa mitaa na vijiji hakikisheni munatambua wageni wote wanaoingia katika maeneo ya utawala pamoja

na kufuatilia shughuli wanazozifanya” Amesema Mhe. Senyamule.


Tukio hilo lilitokea Februari Pili 2024 wakati Timu ya Mkoa ilipofika katika vituo vya Taasisi hiyo vilivyopo

maeneo ya Nkuhungu na Chihanga baada ya kupata taarifa ya uwepo wa vituo hivyo na kubaini baadhi

ya watoto ambao wametoka Dodoma na mikoa ya jirani kama vile Arusha na Manyara kupatiwa

mafunzo hayo.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)