DKT. BITEKO AWASILI MBEYA KWA ZIARA YA KIKAZI

MUUNGANO   MEDIA
0



Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt.Doto Biteko, leo amewasili mkoani Mbeya

kwa  ziara ya kikazi mkoani humo.

Ziara hiyo pia itahusisha ukaguzi wa miradi mbalimbali ya umeme mkoani humo.

Akiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe, Dkt. Biteko amepokelewa na

viongozi mbalimbali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera.

Katika kikao chake na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Dkt. Biteko ameeleza jitihada zinazofanywa

na Serikali katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu, Siasa na Nishati.

Katika Sekta ya Nishati, Dkt. Biteko ameeleza kuwa, upungufu wa umeme nchini ni kati ya

megawati  300 hadi 190 lakini kwa sasa kuna matumaini makubwa kwani mradi wa Julius

Nyerere ( JNHPP) unatarajiwa kuingiza megawati 235 katika gridi ya Taifa mwezi huu na

matumaini mengine ni kutoka Mradi wa umeme wa Rusumo ambao utaingiza katika gridi

megawati 27.

Amesema kuwa, kiasi hicho cha umeme kitakapoingia kwenye gridi ya Taifa kitaondoa hali ya

sasa ya mahitaji ya umeme kuwa makubwa kuliko uzalishaji na pia kuiwezesha Serikali 

kuendelea kufanya maboresho kwenye miundombinu ya umeme.

Amesema kuwa, kwa Mkoa wa Mbeya ambao mahitaji yake ni kati ya megawati 70 na 74

ambapo kwa sasa wanapata umeme wa megawati 51 na kueleza kuwa, jitihada zinazoendelea

sasa zitapelekea Mkoa huo pia kupata umeme kulingana na mahitaji.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amepongeza Mkoa wa Mbeya kwa kufanya vizuri katika

ukusanyaji wa mapato, utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na usimamizi  mzuri wa

sekta Elimu ambao watoto wanaostahili kwenda shule wameripoti kwa zaidi ya asilimia 70.

Vilevile, Dkt. Biteko amesisitiza viongozi kufuata agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuwa, tofauti ya itikadi ya vyama vya siasa  isifanye

wananchi kuwa maadui bali watu wabishane kwa hoja huku kipaumbele kikiwa ni maendeleo ya

nchi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera, amemueleza Dkt. Doto Biteko

kuwa, shughuli za kiuchumi katika Mkoa huo zinaendelea vizuri na katika mwaka 2023/2024

walifanikiwa kukusanya mapato ya shilingi Bilioni 49 ikiwa ni zaidi ya asilimia 105.


Ameongeza kuwa, utekelezaji wa miradi ya umeme inaendelea vizuri ikiwemo ya upelekaji

umeme vijijini, vitongojini na migodini.

Katika elimu amesema kuwa, Mkoa huo umekuwa na ufaulu mzuri huku watoto wanaopaswa

kwenda shule, wakiripoti kwa zaidi ya asilimia 70.


Caps

moja

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akisalimiana na Mkuu wa 

Mkoa wa Mbeya Juma Homera mara baada ya kuwasili  kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa

wa Songwe Februari 19, 2024.

Mbili

Naibu waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto  Biteko, akisalimiana na viongozi

mbalimbali wa mkoa wa Mbeya, mara baada ya kuwasili kwa ziara ya kikazi mkoani humo.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)