ZAIDI YA WANANCHI 45,000 DODOMA WAELIMISHWA ATHARI ZA RUSHWA KUPITIA KAMPENI YA ULIPO TWAJA.

0

 



Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma

 

Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa nchini[TAKUKURU] Mkoa wa Dodoma imeanzisha kampeni maalum ya uelimishaji  kwa jamii dhidi ya madhara ya rushwa ijulikanayo  "ULIPO TWAJA" ambayo uwafuata wananchi waliopo kwenye mikusanyiko na kuwaelimisha masuala ya ubadhilifu na rushwa ambapo hadi sasa wananchi takribani 45,000 wameelimishwa kwenye mikusanyiko 88 ndani ya mkoa wa Dodoma .

 Akizungumza na waandishi wa habari leo Machi,2,2022  jijini Dodoma  Mkuu wa TAKUKURU  mkoa wa Dodoma Sosthenes Kibwengo amesema uelimishaji huo ulianza Januari 18 mwaka huu unalenga kuwafikia wananchi ambao wapo kwenye mikusanyiko mbalimbali.

 

Amesema hiyo ni katika utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan ambapo aliagiza TAKUKURU ijikite Zaidi kuzuia ubadhilifu kabla haujatokea katika miradi ya maendeleo.

“Tunawafuata wananchi kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo

 

Amesema mkoa wa Dodoma unakadiriwa kuwa na wakazi 2,729,153 na kwamujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 asilimia 52.2 ya watanzania ni wale wa rika la miaka 15 hadi 64 hivyo katika kampeni hiyo ya ULIPO TWAJA Takukuru Mkoa wa Dodoma imekusudia kuwafikia angalau asilimia 10 ya wananchi wa rika hilo ambao ni takribani wakazi 142,461.

 

 

Ameeleza kuwa wao kama Taasisi ya kuzuia na kupamabana na rushwa wameona uelimishaji huo ni sahihi kwani utawafikia wananchi wanatumia muda mwingi katika shughuli za kujipatia riziki zao masokoni,Vituo vya bajaji na bodaboda vijiwe vya kahawa au wale ambao wanaenda kupata huduma kama mikusanyiko ya wanufaika wa TASAF, siku za lishe kwenye Vituo vya afya, siku za kliniki au chanjo,stendi za daladala na mabasi,Nk.

 

"Lengo la kampeni hii ni kuwafikia wananchi ambao kulingana na aina ya kazi au Biashara wanazofanya sio rahisi kuwapata kwenye mikutano ya hadhara au mikutano mingine rasmi kama ya Vijiji na Mitaa inafahamika wazi wengine uendeshaji wa maisha yao hutegemea uwepo wao katika maeneo hayo yamikusanyiko hivyo sio rahisi kuondoka na kuacha shughuli zao ili wahudhurie mikutano ya hadhara ,"amesema Kibwengo.

 

Aidha amesema  iwapo mkusanyiko husika utakuwepo saa 12 asubuhi  basi ULIPO TWAJA itawafuata na kuwaelimisha hata kama mkusanyiko  huo utakuwa mchana au njioni .

 

Akiwa katika eneo la uelimishaji soko la Bonanza jijini Dodoma Afisa Uchunguzi Dawati la Elimu kwa Umma TAKUKURU  Sabeth Mshana amesema katika kuelekea siku ya wanawake Duniani Machi,8,2022 wameamua kujikita Zaidi kuelimisha wanawake juu ya manyanyaso wanayopata ikiwemo rushwa ya ngono huku Mkuu wa uelimishaji TAKUKURU mkoa wa Dodoma Faustine Malecha  akiwataka wanawake kuwa majasiri katika mapambano ya rushwa.

Akizungumza baada ya kupata elimu hiyo ya Rushwa ,mmoja wa wafanyabiashara jijini Dodoma Belice Malima amesema elimu ya rushwa ina umuhimu mkubwa katika jamii

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)