WIZARA YA AFYA YATOA TAHADHARI KUHUSU MLIPUKO WA UGONJWA WA HOMA YA MANJANO ULIORIPOTIWA NCHINI KENYA.

0

 



Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.

Kutokana na ugonjwa wa homa ya manjano kuripotiwa nchini Kenya  Machi,3,2022  katika Kaunti ya Isiolo  kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na shirika la Afya Duniani [WHO]. Wizara ya Afya imetoa tahadhari kwa wananchi kujikinga na ugonjwa huo.

Hayo yamesemwa leo Machi 9,2022 na waziri wa Afya Ummy Mwalimu wakati akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dodoma  amesema kuna tetesi zingine kutokea nchini Uganda hivyo wizara ya Afya imejipanga kudhibiti ugonjwa huo ambapo baada ya uchunguzi wa wizara bado ugonjwa haujaingia nchini .

Waziri Ummy   ameanisha miongoni mwa dalili za ugonjwa wa homa ya manjano kuwa ni pamoja na kutokwa damu puani,kuumwa na kichwa.

 

AidhaWaziri Ummy ametaja nchi barani Afrika zilizo hatari kukumbwa na  wimbi la  ugonjwa wa homa ya manjano kuwa ni pamoja na Angola, Benin ,Burkina faso ,Burundi,Cameroon,Jamhuri ya Afrika ya kati,Chad,Ivory Coast DRC Congo ,Guine Ikweta ,Gabon,Gambia,Guine,Guine Bissau,Kenya ,Liberia .Mali,Mauritania,Niger,Nigeria,Rwanda,Senegal,Sierra Leone ,Sudan Kusini,Togo,na Uganda.

Hata hivyo,ameanisha mikakati ya Wizara katika mapambano ya ugonjwa huo ni pamoja na kuchanja kwa wasafiri ambapo kwa nchi za Afrika mashariki gharama za chanjo ni Tsh.30,00 huku akiagiza wataalam wa afya kwenda mipakani katika kuhakikisha mtu anayeingia nchini  kutoka nchi zenye idadi kubwa ya watu wenye ugonjwa huo wanachanjwa homa ya manjano.

Mwakilishi  Mkaazi wa shirika la Afya Duniani   [WHO]Dkt.Tigest  Katsela  Mangestu amesema asilimia 60 ya wagonjwa wa homa ya manjano hufariki dunia huku akibainisha sababu za kuitwa homa ya manjano ni kutokana mwili  pamoja na macho kuwa na rangi ya njano.

 

Ikumbukwe kuwa ,katika nchi za Afrika Mashariki, Tanzania haijawahi kuwa na taarifa ya mgonjwa yeyote aliyethibitika kuwa na ugonjwa wa Homa ya Manjano tangu mwaka 1950

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)