RC MTAKA AGOMEA ANDIKO LA UJENZI WA STENDI BAHI.

0

 



Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma ,

Mkuu wa mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka ameiagiza halmashauri ya Wilaya ya Bahi kufuta andiko la ujenzi wa kituo cha mabasi kwa Tsh.Milioni 20  kwani kiasi hicho akiendani na hadhi ya halmashauri .

Mtaka amebainisha hayo Wilayani Bahi katika mwendelezo wa ziara yake  kuhusu maelekezo ya Rais ukamilishaji anwani za makazi na posti kodi,kuhamasisha kiwango cha ufaulu pamoja na kuinua kiwango cha uchumi kwa kuibua miradi mbalimbali bunifu ya maendeleo .

Mkuu huyo wa mkoa amesema Bahi ndio lango kuu la Kuingilia makao makuu jijini Dodoma hivyo haiwezekani kujenga  kituo cha mabasi kwa kiwango cha chini cha Tsh.Milioni 20

“Milioni 20 stendi ya kwa hadhi ya Bahi,Milioni 20 ni stendi ya kata moja kubwa,Bahi ndio Gateway ya Makao makuu ,Bahi ndio Kibaha ya Dar Es Salaam tunataka kuona Mbezi kama Kimara Mwisho,PHD ,Degree mnakaa mnakubaliana kujenga stendi ya  Tsh.milioni 20 mtachekwa hadi na mbwa”alisisitiza Mkuu huyo wa mkoa.

Aidha,Mkuu huyo wa Mkoa amesema haiwezekani Wilaya ya Bahi iwe na maeneo mazuri ya kilimo halafu wananchi wake wawe masikini na tegemeo katika mikoa jirani hivyo ameagiza Februari ,28,2022  kukutana na skimu zote 16  za umwagiliaji  katika kuleta mapinduzi ya kilimo huku pia akiagiza kuongeza kasi ya upimaji wa ardhi na kumtaka mkurugenzi  wa Bahi kwenda kujifunza Kahama jinsi maeneo ya kimkakati yalivyopangwa.

Kuhusu suala la elimu ,Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mwanahamis Mkunda amesema wilaya yake imeweka mikakati mbalimbali kuhakikisha kiwango cha ufaulu kinaongezeka.

Nao baadhi ya Madiwani kutoka kata za Wilaya ya Bahi akiwemo Blandina Magawa diwani wa Ibugule,Anthony Lyamunza diwani wa Makanda pamoja na Sosthenes Mpandu diwani wa Mpamantwa wamesema watahakikisha wanashirikiana na  Watumishi wa Halmashauri katika kuchangia mawazo chanya kwa maendeleo ya Bahi

Akiwa ziara   katika halmashauri ya Kondoa Mjini mkuu huyo wa Mkoa alikutana na makundi mbalimbali ya watumishi wa halmashauri na kusikiliza kero zao akiwemo Afisa Ugavi halmashauri ya Kondoa Mjini kutokuwa na maelewano mazuri na Mkurugenzi  wa halmashauri hiyo Paul Sweya.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka aliwataka watumishi wa halmashauri ya Kondoa Mjini  kuacha mivutano na badala yake  wawe  na mshikamano   na kuwa wabunifu kwa kuibua miradi  bunifu na  ya kimkakati itakayosaidia kuleta maendeleo  na kuvutia wawekezaji.

“Mnagombana kwa sababu hamna ajenda ,mkurugenzi kata nane unashindwa kupanga mipango madhubuti inakuwa halmashauri ya mfano,unaweza ukaamua

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kondoa  mji Mohammed Kiberenge anaahidi kuitisha kikao cha dharura cha baraza la madiwani kusuluhisha mgogoro huo baina ya Mkurugenzi na Afisa Ugavi.

 

Katika hatua nyingine Mtaka aliziagiza halmashauri kuja na mkakati wa kutunga sheria ndogo zitakazosaidia kuwabana watu waharibifu wa miundombinu ya anwani za makazi na postikodi

Mtaka alitoa maagizo hayo  wakati akizindua zoezi la uwekaji wa mfumo wa anwani za makazi na postikodi katika barabara ya Iboni halmashauri ya Kondoa  .

 

Mkuu huyo wa Mkoa alisema haiwezekani serikali kuwekeza fedha nyingi katika utekelezaji wa mifumo ya anwani za makazi na postikodi halafu ajitokeze mtu kuharibu miundombinu kwa kuuza kama chuma chakavu.

Akizungumzia  katika utekelezaji  wa zoezi la mfumo wa anwani za makazi na postikodi ,mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Kondoa Paul Sweya amesema jumla ya barabara 255 zilibainishwa kwa kupewa majina  ambapo halmashauri imeandaa mabomba 230,na vibao 255 vya mitaa huku mkuu wa Wilaya ya Kondoa ,Dkt.Khamis Mkanachi akisema zawadi kwa Rais ni kukamilisha zoezi hilo mapema kabla ya muda uliopangwa ambao ni Mei,2022.

 

Katika hatua nyingine mkuu wa mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka alitembelea shule ya wasichana Kondoa katika kuhamasisha suala la elimu.

 Mtaka amezitaka kamati za taaluma mkoani Dodoma kukaa pamoja kuwaandaa vyema wanafunzi walio kwenye madarasa yenye mitihani ya kitaifa ili kuwaandaa kufanya vyema wanafunzi katika mitihani yao.

 

Mkuu huyo wa Mkoa alisisitiza kuwa Kila  ufaulu wa A,kwa  matokeo kidato cha sita Ofisi ya mkoa itagharamia kwa Tsh.Elfu thelathini[30,000],na shule itakayoingia 10 bora itapewa milioni 5 huku kila A kwa matokeo kidato cha nne itagharamiwa  Tsh.20,000.

 

Hivyo aliwataka wanafunzi kusoma kwa bidi kwa manufaa yao wenyewe na serikali imewekeza gharama kubwa katika shule hiyo.

 

 







Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)