WAANDISHI WA HABARI WANNE MBARONI KAHAMA KWA KUJIPATIA FEDHA KIUDANGANYIFU KWA KUDAI KUWA NI MAAFISA USALAMA WA TAIFA

0

 Tokeo la picha la mahakamani leo


Wakazi wanne mjini  Kahama leo wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya  Kahama kwa tuhuma ya  kujiwakilisha kama watumishi wa serikali na kujipatia fedha kwa njia udanganyifu.

Watuhumiwa hao ni  Paul Kayanda[36} mkazi wa Majengo ,Shaban Njia [26] mkazi wa Nyahanga,Simon Dioniz [42] na Raymond Mihayo[42] Mihayo  wote wanatuhumiwa kwa madai ya  kujiwakilisha kama watumishi wa serikali  maafisa wa usalama wa taifa  na kujipatia fedha kiasi cha shilingi milioni moja kutoka kwa mkazi mmoja mkazi wa Banhi wilayni Kahama.

Mbele ya  Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo Keneth Mtembei ,mwendesha mashtaka  Zuberi Mateso wamedai kuwa watuhumiwa walikamatwa na jeshi la polisi  Januari 9 mwaka huu nyumbani kwa  Jane Mbeshi [46]  mganga wa jadi kwa kumtuhumu kufanya ramli chonganishi na kudai awape fedha hizo.

Washtakiwa hao ambao wanadaiwa kuwa waandishi wa habari kutoka mjini Kahama wamekana  mashtaka yote mawili na kurudishwa rumande kwa kukosa dhamana hadi Januari 24 mwaka huu shauri lao litakapotajwa tena.

Kamanada wa polisi mkoani Shinyanga Simon Haule amesema kuwa Shaban Njia,Raymond Mihayo,Paulo Kayanda na Simon Dioniz na mwingine George Maziku  ambaye  bado anatafutwa na Jeshi la Polisi hilo Januari 6 Mwaka huu walijiwasilisha kwa Mbeshi na kudai kuwa ni maafisa Usalama wa Taifa na kudai wapatiwe pesa.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)