
Mbunge wa Msalala,Ezekiel Magolyo Maige
Mbunge wa jimbo la Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga Ezekiel Maige ameahidi kutoa mifuko 50 ya saruji katika ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Nyamishiga kata ya Lungunya halmashauri ya Msalala.
Mbunge wa jimbo la Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga Ezekiel Maige ameahidi kutoa mifuko 50 ya saruji katika ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Nyamishiga kata ya Lungunya halmashauri ya Msalala.
Akizungumza
katika mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji hicho Maige amesema kuwa msaada huo alioutoa ni
kuunga mkono juhudi za wananchi katika
shughuli za maendeleo.
Hata hivyo Maige ameagiza kuorodheshwa dawa zote
zinazotakiwa kutolewa katika vituo vya afya ili wananchi waweze kufahamu kwani kuna baadhi ya dawa hutolewa bure na kutokufahami hilo watumishi wa afya hutumia mianya hiyo kuuza dawa zilizotolewa ruzuku na serikali ili ziwanufaishe wananchi.
Aidha
Mbunge huyo amewataka wananchi kukata bima ya CHF iliyoboreshwa ili wapate Bima
kwa ajili ya matibabu kwa gharama nafuu, huku akiwataka wazee pia wenye umri kuanzia miaka 60 na kuendelea
kujiandikisha ili nao waweze kupata bima bure.
Katika
hatua nyingine Mmoja wa wakunga wa jadi wa kijiji cha Nyamishiga Selema
Ndelembi amelalamikia suala la wakunga kijijini hapo kutolipwa licha ya kazi kubwa wanazofanya za kuwasaidia akina mama wajawazito
kuwapeleka hospitalini kujingufungua .
Akilitolea
ufafanuzi suala hilo diwani wa kata ya Lunguya Benedict Musa Manuary amesema
kuwa suala la wakunga wa jadi ni uzembe na
ukiritimba wa watumishi wa Afya akiwemo mganga wa kituo cha Afya cha
Lunguya na kuongeza kuwa wakunga
wanmekuwa na mchango mkubwa wa kuokoa uhai wa wajawazito wanaojifungulia
majumbani hata nyakati za usiku.
Ziara ya
Mbunge Maige imeanza leo katika kata ya
Lunguya ambapo amefanya mikutano miwili ya hadhara katika vijiji vya Nyamishiga
na Madaho katika halmashauri ya Msalala.