BUYOZI KAHAMA WAKUMBWA NA CHANGAMOTO YA BARABARA YA BUYOZI MWAKATA

0


            
Wakazi wa kijiji cha Buyozi kata ya Mwakata halmashauri ya Msalala Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga wamelalamikia ubovu wa miundo mbinu ya barabara ya Buyozi Mwakata hususan  kipindi hiki cha masika.
                                                                 
Wakizungumza na Gimu Blog spot kijijini hapo  baadhi ya wakazi hao wamesema kuwa ubovu wa barabara hiyo  kimekuwa ni kikwazo cha kukwamisha shughuli mbalimbali za maendeleo.

Hivyo wameiomba serikali kusaidia kukarabati barabara hiyo kwa kuweka changalawi na kuongeza madaraja kutokana na eneo kubwa la barabara hiyo kuwa la mbuga.



Kwa upande wake Diwani wa kata ya Mwakata Ibrahim Six Masanja amewataka wananchi wa Buyozi kuwa na subira kwani tayari kuna mkandarasi ameshapatikana kupitia wakala wa barabara vijijini na mtaani TARURA

Na.Faustine Gimua              Chanzo:Mahojiano.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)