MABOMA YA ZAMANI MSALALA YAWEKEWE KIPAUMBELE=MADIWANI

0
Baraza la madiwani la halmashauri ya Msalala Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga limeiomba halmashauri hiyo kuyawekea kipaumbele cha kwanza maboma yaliyokaa kwa muda mrefu bila kupauliwa ili yaweze kukamilika hali itakayoondoa migogoro ya wananchi baina yao na wawakilishi wao.

Wakizungumza katika kikao cha kujadili bajeti kwa mwaka wa fedha 2018/2019 diwani wa kata ya Mwalugulu Flora Sagasaga na diwani wa Kata ya Ikinda Matrida Musoma, wamesema kuwa ni vyema bajeti ikajikita kusaidia kata zao kwanza kutokana na changamoto zilizopo.

Akijibu hoja hizo Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Msalala ambaye pia ni mhasibu wa halmashauri hiyo Masatu Mnyoro amesema kuwa wananchi hawana budi kuendelea kuwa na uvumilivu.

Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Msalala Ezekiel Maige amesema ni vyema kushirikiana na idara ya Afya kufanya tathmini ya maboma ya zahanati ili na mengine yakamilike huku pia akitoa wito kwa halmashauri ya Msalala kuwa na mpango madhubuti ya matumizi ya fedha.








Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)