BARAZA LA MADIWANI MSALALA LATAKA SHULE ZOTE ZA BWENI ZIPEWE RUZUKU ILI KUONDOA MKANGANYIKO WA MCHANGO

0
:RUZUKU
Baraza la madiwani halmashauri ya  Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga limeomba serikali kuu kuziingiza kwenye mfumo wa ruzuku shule za bweni  ambazo hazimo kwenye mfumo huo ili kuondoa mkanganyiko wa kuchangia chakula shule hizo.

Wakizungumza katika kikao cha baraza hilo,Mwenyekiti wa halmashauri ya Msalala Mibako Mabubu na diwani wa kata ya Ikinda Matrida Musoma wamesema kuwa kati ya shule 5 za mabweni  ni shule moja tu inayopewa ruzuku na serikali huku zingine ni makubaliano na wazazi.

Makubaliano ya wazazi  kuchangia chakula shuleni yanatokana na shule hizo kuwa mbali hivyo waliamua kufanya hivyo ili kuzuia mimba shuleni kutokana kutembea umbali mrefu.
Aidha wameongeza kuwa ili kuondoa mkanganyiko huo ni vyema serikali ikaziingiza kwenye mfumo wa ruzuku shule zote  5 za sekondari za bweni zilizopo katika halmashauri hiyo na kama haina uwezo iendelee kuruhusu michango.

 Shule za sekondari  ambazo zipo kwenye mfumo wa bweni  lakini hazimo kwenye mfumo  wa ruzuku ni Chela,lunguya,busangi na Isaka na Shule iliyo kwenye mfumo wa ruzuku ni Mwalimu Nyerere huku Ntobo na Bulige zikiwa katika hatua ya Mwisho ya ukamilishaji na kuwa za bweni.

Katika hatua nyingine mwenyekiti wa halmashauri ya   Msalala  Mibako Mabubu ameitaka  Wakala wa barabara vijijini TARURA  kuwa karibu na halmashauri hiyo ili kufanyakazi kwa ufanisi zaidi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)