VIJANA 12 KAHAMA WAACHA UTUMIAJI WA DAWA ZA KULEVYA NA KUHUDHURIA NYUMBA ZA IBAADA

0
Jumla ya vijana 12  wanaoishi katika mazingira hatarishi mjini Kahama  wameamua kuacha matendo maovu na kuanza kuhudhuria kwenye  nyumba  ya ibaada katika kanisa la waadventista wasabato Kahama mjini.
Wakizungumzia juu ya kubadilika tabia na kuachana na matendo maovu wakiwa kanisani hapo vijana hao wamesema kuwa maisha yao hapo awali yalikuwa ni utumiaji wa madawa ya kulevya pamoja na  wizi .

Mmoja wa wazee wa kanisa la wasabato Kahama Mjini Wilson Peter amesema kuwa vijana hao wameendelea kupokea wito na kubadilika kuwa na matendo mazuri.

Naye mmoja wa vijana  Sabato Mwita  ambaye kwa sasa anaishi katika maisha mazuri  Sabato Mwita amewatia moyo vijana kuendelea kubadilika kwani naye alipitia  maisha hatarishi ya mtaani lakini imebaki kuwa historia .

Licha ya kanisa la waadventista wasabato Kahama mjini kupokea vijana 12 waliokuwa wanatumia madawa ya kulevya limeshiriki meza ya bwana ambapo mmoja wa wazee wa kanisa hilo Petrol Kakenele   amesema kuwa meza ya bwana humuweka mtu karibu na Mungu  na pia ni kielelezo cha ushirika na yesu Kristo.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)