JAMII WILAYANI KAHAMA YATAKIWA KUTOA TAARIFA PANAPOTOKEA VITENDO VYA KIKATILI

0




 
 PICHA KUTOKA MAKTABA
Jamii wilayani kahama mkoani shinyanga imeaswa kutoa taarifa katika mamlaka husika wanapoona vitendo vya ukatili kwa watoto vikitendeka.

Hayo yamesemwa na mwanasheria kutoka shirika la msaada wa kisheria lililopo wilayani Kahama KAHAMA PARALEGAL ORGANIZATION (KAPAO) Bi Upendo Erisha Mahobe wakati akizungumza na Gimu Blog.

Amesema kuwa kutengana kwa wazazi ni tatizo kubwa ambalo linasababisha watoto wengi kukubwa na ukatili wa aina mbalimbali wawapo mtaani.

 Aidha amesisitiza kuwa wazazi wanapotengana baba anajukumu la kutoa mahitaji yote ya muhimu anayopaswa kupatiwa mtoto  hivyo  wanapaswa kufuata sheria inavyoelekeza.

Katika hatua nyingine  amewataka watoto wasifumbie macho vitendo  vyote vya kikatili wanapofanyiwa kwani wanajukumu la kutoa taarifa pia.

Pamoja na hayo ametumia nafasi hiyo kuitaka jamii kuelewa haki za watoto na kuzijua sheria zinazowalinda watoto wote ili kuwalinda dhidi ya ukatili katika jamii.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)