VETA YATAKIWA KUENDELEA KUWASHIRIKISHA WATAALAM WALIOBOBEA KATIKA FANI MBALI MBALI.

MUUNGANO   MEDIA
0


 Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imetakiwa kuendelea kuwashirikisha wataalamu waliobobea katika fani mbalimbali zinazotolewa vyuoni, ili kuwezesha mafunzo kwa vitendo na kujenga umahiri kwa vijana.


Rai hiyo imetolewa Agosti 15, 2026 jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Mhe. Husna Sekiboko, akisema ushirikishwaji huo utawawezesha vijana kupata ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira na jamii.



Amesema vyuo vya VETA havipaswi kujifungia kama kisiwa, wataalamu kutoka Jeshi la Zimamoto, maafisa biashara na sekta nyingine zinaweza kushirikishwa kulingana na mahitaji ya fani.


Mhe. Sekiboko ameipongeza Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutekeleza Ilani ya Uchaguzi kupitia ujenzi na uimarishaji wa vyuo vya VETA, hatua inayolenga kuwawezesha vijana kupata ujuzi na fursa za ajira na kujiajiri.


Aidha, Mwenyekiti huyo amepongeza uanzishwaji wa kampuni tanzu za VETA zinazolenga kuongeza uzalishaji wa bidhaa halisi badala ya vielelezo pekee hatua itawawezesha wanafunzi kujifunza kwa vitendo, kuongeza mapato ya vyuo na kuwajengea vijana uwezo wa kibiashara.





Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)