Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, awasili Bungeni jijini Dodoma leo Mei 22, 2026 kwa ajili ya kuwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa mwaka wa fedha 2026/2027.
Waziri Kapinga anatarajiwa kuwasilisha vipaumbele vya wizara hiyo vinavyolenga kuimarisha sekta ya viwanda, kukuza biashara ya ndani na nje ya nchi pamoja na kuongeza mchango wa sekta hiyo katika uchumi wa taifa.
Aidha, hotuba hiyo inatarajiwa kueleza mipango ya Serikali katika kuvutia uwekezaji, kuongeza ajira kupitia viwanda na kuboresha mazingira ya biashara nchini.
