USAFI WA MAZINGIRA HUZUIA MAGONJWA YA MLIPUKO.

MUUNGANO   MEDIA
0

 TAZAMA VIDEO HAPA CHINI



Na. Elimu ya Afya kwa Umma.

 Katika utekelezaji wa kampeni ya mtu ni afya,wito umetolewa kwa wakazi wa jiji la dodoma kujenga tabia ya kufanya usafi mara kwa mara katika maeneo yanayowazunguka ili kujikinga na magonjwa ya mlipuko.

 Wito huo umetolewa Jijini Dodoma na Mkuu wa Kitengo cha Usafi na Mazingira Halmashauri ya Jiji la Dodoma Dickson Kimaro wakati wa zoezi la Uhamasishaji kufanya usafi katika jiji hilo.

 Mwenyekiti wa vikundi vya Usafi Halmashauri ya Jiji la Dodoma  Seleman Sanya amesema ni muhimu kuzingatia usafi wa mita tano kila upande katika mazingira yanayokuzunguka.

 Nao baadhi ya wananchi Jijini Dodoma akiwemo Anna Jonas wamesema wameitikia wito wa kufanya usafi katika kuyaweka mazingira katika hali ya usafi ili kuzuia vimelea vya magonjwa.

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)