UMEWAHI KUJIULIZA KUWA MTANDAO UNAKWAMISHA SHUGHULI ZA KIUCHUMI? 

MUUNGANO   MEDIA
0

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977,Ibara  ya 18Kifungu kidogo cha pili inaeleza kuwa Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbali mbali nchini na Duniani  kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia juu ya masuala muhimu kwa  Jamii.

Suala hili linadhihirisha kwamba mtandao wa Intanenti ni muhimu katika suala zima la mawasiliano katika ulimwengu huu wa Sayansi na Teknolojia.

Kukosekana kwa huduma za mtandao,upatikanaji wa intaneti unazuiliwa au kuzuiliwa kwa muda fulani, ni suala linalozidi kuwa na athari kubwa katika jamii zetu za kidijitali katika baadhi ya nchi za afrika.

Kutokana na hili baadhi ya Vijana na wanawake wametoa ushauri kwa wafanyamaamuzi na wanaharakati kuhakikiksha  wanasimamia suala la  mtandao kuhakikisha Mawasiliano ya mtandao yanakuwa  huru wakati  wote hasa katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kudai kuwa ni haki  yao ya msingi.

Wameeleza kuwa wakati uliopo sasa ni wa Kidijitali kutokana na Dunia kuwa Kijiji  ambapo mawasiliano ya mtandao yanatumika  kuendesha shughuli mbalimbali za maendeleo na kama Vijana kwao inakuwa ni tatizo kutokana na kukosa Fursa za kazi na biashara kupitia mitandao.

Sanjari na hilo wameomba Elimu zaidi  iendeleeebkutolewa kwa jamii kuhusu athari za kuzimwa kwa mtandao  kwa manufaa ya Taifa.

Tumeshuhudia kuwepo kwa taarifa mbalimbali kupitia Mitandao ya kijamii ikiwemo Fursa za Ajira  Pamoja na sponsa za masomo hivyo ni muhimu suala la mtandao likapewa kipaumbele kama zilivyo huduma nyingine za kijamii kama Maji,Afya nakadhalika.

Kutokana na kutangazwa kwa nafasi za Ajira na Jeshi la Polisi Nchini Mei10 Mwaka 2024 taarifa  zimesambaa kutokana na kuwepo kwa Mitandao wa Intaneti  ambao vijana wameonekana kuchangamkia fursa wengine kuwepo katika sehemu za kutolea huduma za mitandao ya Internt (Internet Cafe) lakini kukosa huduma .

Kukosekana kwa huduma ya mtandao wa intaneti imetokqna na hitilafu ya kiteknolojia na kusababisha  

Kituo hichi kimewashujudia vijana hao na kuzungumza nao  juu ya umuhimu wa internet ambapo wamesema  suala la matumizi ya internet ni muhimu kwa tija Zote kwani Ni Nyanja ya kiuchumi.

“Naomba haya tu atakuwa kutuma kwa njia ya mtandao lakini kuwepo kwa tatizo lakukosekana kwa mtandao imesababisha kushindwa kutuma maombi tovuti haifunguki hivyo ni tatizo kwetu nakuomba Serikali kuongeza muda wa maombi,””Wamesem

Hata hivyo baadhi ya wafanyabiashara kwanjia ya mtandao wamesema kutokana na hitilifu ya Kukosekana kwa huduma ya mtandao wa intaneti umewasababishia hasara kutokana na huduma hiyo kukosekana.

Mnamo mei 12 Mwaka 2024 Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Ulifika taarifa kuwepo kwa tatizo la mtandao nchini na kuahidi kuishughulikia changamoto hiyo.

MWISHO

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)