MUUNDO WA NEMC KUWA MAMLAKA WASHIKA KASI

MUUNGANO   MEDIA
0


 Serikali imeanza kufanya marekebisho ya kubadili muundo wa Baraza la

Taifa na Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na kuwa Mamlaka

ya Usimamizi wa Mazingira (NEMA).

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe.

Khamis Hamza Khamis amesema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa

Viti Maalumu Mhe. Maryam Azan Mwinyi aliyetaka kujua ni lini Serikali

itawasilisha Marekebisho ya Sheria ya Mazingira ili kuipa NEMC uwezo

wa hadhi ya Mamlaka.

Amesema kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais inatarajia kuwa hadi

kufikia Juni 2024, Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa

Mazingira Sura 191 uwasilishwe katika Bunge la Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania kwa hatua zaidi.

Akiendelea kujibu swali hilo Naibu Waziri Khamis amesema kuwa

marekebisho hayo ya kubadili muundo huo ni moja ya

masuala yanayopendekezwa kufanyiwa marekebisho ili NEMC iwe

Mamlaka. 

Akiendelea kujibu maswali ya nyongeza ya mbunge huyo, Mhe. Khamis

amesema kuwa miongoni mwa majukumu ya mameneja wa kanda wa

NEMC ni kusimamia sheria pamoja na kutoa elimu kwa jamii.

Ametumia nafasi hiyo kuwapongeza kwa utendaji kazi mzuri na kusema

kuwa majukumu hayo yanaweza kufanyiwa marekebisho kulingana na

sheria itakavypendekeza.

Hivyo, Naibu Waziri Khamis amesema kuwa NEMC itakayofahamika kama

NEMA itaendelea kushirikiana kwa ukaribu na Mamlaka ya Usimamizi wa

Mazingira (ZEMA) katika utekelekezaji wa majukumu ili usimamizi wa

mazingira nchini uwe endelevu na wenye mafanikio.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)