MAWAZIRI SJMT NA SMZ WAKUTANA ZANZIBAR

MUUNGANO   MEDIA
0



 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SJMT) na Serikali ya Mapinduzi

ya Zanzibar (SMZ) zimefanikiwa kutatua hoja 21 za Muungano kati ya 25

zilizokuwepo awali.

 

Waziri Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dk. Selemani

Jafo amesema hayo katika Kikao cha Mawaziri wa SJMT na SMZ cha

kujadili Masuala ya Muungano kilichofanyika Nyamanzi, Zanzibar leo Machi 05,

2024

Amesema kuwa tangu mchakato wa kutatua changamoto hizo ulipoanza, hadi

sasa zimebaki hoja nne za Muungano ambazo Serikali zote mbili zinaendelea

kuzitafutia ufumbuzi.

Dkt. Jafo ambaye ni Mwenyekiti Mwenza wa kikao hicho amesema viongozi wa

pande zote mbili za Muungano wamekaa pamoja kujadili hoja hizo nne za

Muungano zilizobaki na kuangalia namna ya kuzipatia ufumbuzi.

 

Amezitaja hoja nne zilizobaki kuwa ni pamoja na Suala la Sukari, Usajili wa

Vyombo vya Moto, Bodi ya Pamoja na Mgawanyo wa Mapato ya iliyokuwa

Sarafu ya pamoja ya Afrika Mashariki.

 

Kutokana na mafanikio, Dk. Jafo amewapongeza Rais wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar

na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.Hussein Ali Mwinyi kwa kazi

kubwa wanayoifanya katika kutatua hoja zilizobaki.

“Niwapongeze pia Mawaziri, Makatibu Wakuu na Wataalamu mbalimbali

kutoka Serikali za pande zote za Muungano kwani wamefanya kazi kubwa ya

kuchakata changamoto zilizokuwepo hadi kufikia mafanikio haya,“ amesema

Dkt. Jafo.

 

Kwa upande Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili ya Rais (Sera, Uratibu na

Baraza la Wawakilishi) Mhe. Hamza Hassan Juma amesema kuwa lengo la

kikao hicho ni kuzungumzia hoja mbalimbali zinazokabili utendaji wa shughuli

za SJMT na SMZ.

 

Amesema kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar umedumu kwa muda

mrefu kutokana viongozi wa pande zote mbili za Muungano kukaa pamoja na

kujadili changamoto zinazojitokeza kwa uwazi na kuzipatia ufumbuzi kwa

pamoja.

 

Akitolea mfano wa mafanikio ya Muungano huu, Mhe. Hamza amesema

Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) inayoundwa na nchi nane inaendelea

kudumu kutokana na uzoefu unaopatikana Tanzania na hivyo jumuiya hiyo

kuendelea kukua.


 

Ameongeza kuwa hoja nyingi zimeshatatuliwa hivyo mkutano huo unatoa

matumaini makubwa kupatikana kwa maslahi ya wananchi wa pande zote

mbili pamoja na kuendelea kudumisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

ambao unatimiza miaka 60 ifikapo Aprili 26, 2024.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)