RAIS SAMIA ATOA SALAMU ZA POLE MAAFA YA MAFURIKO

0


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan atoa salamu za pole na kutoa maelekezo kwa vyombo vinavyoshughulikia maafa yaliyotokea katika kijiji cha Katesh Wilayani Hanang Mkoani Manyara.

Ni muhimu kila mmoja wetu kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya Mvua kubwa ikiwemo kuacha kupima nguvu ya maji, kuacha kusimama chini ya mti pindi Mvua inaponyesha, kuzuia watoto kucheza kwenye madimbwi au karibu na kingo za mito.

Aidha, ni muhimu kuzuia mlipuko wa Magonjwa ikiwemo Malaria kwa kufukia madimbwi,kutumia chandarua kila unapolala hata mchana na kusafisha Mazingira yote yanayokuzunguka.

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)